Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ukumbusho Unaunganisha Watu wa Mungu

Ukumbusho Unaunganisha Watu wa Mungu

Jinsi ilivyo vyema na jinsi inavyopendeza . . . kukaa pamoja kwa umoja!”​—ZAB. 133:1.

NYIMBO: 18, 14

1, 2. Ni tukio gani lenye kuunganisha zaidi la mwaka wa 2018, na sababu gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

TAREHE 31 Mwezi wa 3, 2018, wakati jua linaanza kushuka, watu wa Mungu na wengine wengi wenye kupendezwa watakutana pamoja kwa ajili ya tukio la kila mwaka la Chakula cha Bwana cha Mangaribi. Mamilioni ya watu watakusanyika pamoja ili kufanya Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Kila mwaka, tukio hilo ndilo lenye kuunganisha sana watu kuliko tukio lingine lolote lenye kufanywa katika dunia!

2 Tunaweza kuwazia namna Yehova na Yesu wanafurahi wakati wanaona mamilioni ya watu katika dunia yote wanakusanyika saa mbalimbali juu ya tukio hilo la pekee mupaka siku hiyo inaisha. Biblia ilitabiri kama ‘umati [ao, mukutano] mukubwa, ambao hakuna mutu [angeweza] kuuhesabu, kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga’ ungesema hivi kwa sauti kubwa: “Wokovu unatoka kwa Mungu wetu, anayeketi juu ya kiti cha ufalme, na Mwana-Kondoo.” (Ufu. 7:9, 10) Ni jambo lenye kupendeza sana kwamba Yehova na Yesu wanaheshimiwa kupitia tukio hilo la Ukumbusho lenye kufanywa kila mwaka!

3. Habari hii itajibia maulizo gani?

3 Habari hii itajibia maulizo yenye kufuata. (1) Namna gani tunaweza kujitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho na kupata faida wakati tunahuzuria? (2) Ni katika njia gani Ukumbusho unachochea umoja kati ya watu wa Mungu? (3) Kila mumoja wetu anaweza kufanya nini ili kuendeleza umoja huo? (4) Kuko siku kutakuwa Ukumbusho wa mwisho; ikiwa ndiyo, wakati gani?

NAMNA YA KUJITAYARISHA KWA AJILI YA UKUMBUSHO NA KUPATA FAIDA

4. Sababu gani ni jambo la maana sana kwetu kuhuzuria Ukumbusho ikiwa inawezekana?

4 Fikiria sababu gani ni jambo la maana ukuwe kwenye Ukumbusho. Kumbuka kuwa mikutano ya kutaniko ni sehemu ya ibada yetu. Kwa kweli, Yehova na Yesu wanaona mutu mwenye kujikaza sana ili kuhuzuria mukutano huo wa maana sana katika mwaka. Kusema kweli, tunapenda waone kama tutakuwa kwenye Ukumbusho kama hakuna matatizo makubwa ya afya ao hali zingine zenye zitatuzuia. Wakati tunaonyesha kupitia matendo yetu kama kukusanyika pamoja ili kuabudu ni jambo la maana kwetu, tunamupatia Yehova sababu ingine ya kuandika majina yetu katika “kitabu cha kumbukumbu,” ni kusema, “kitabu cha uzima,” ambamo majina ya wale wote wenye Yehova anapenda kupatia uzima wa milele yameandikwa.​—Mal. 3:16; Ufu. 20:15.

5. Siku fulani mbele ya Ukumbusho, namna gani tunaweza ‘kujijaribu kama tuko katika imani’?

5 Siku fulani mbele ya Ukumbusho, tunaweza kujipangia wakati wa kusali na kuchunguza kwa uangalifu urafiki wetu pamoja na Yehova. (Soma 2 Wakorintho 13:5.) Namna gani tunaweza kufanya hivyo? Kwa ‘kujijaribu kama tuko katika imani.’ Ili kufanya hivyo, tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Ninaamini kabisa kama niko katika tengenezo moja tu lenye Yehova amekubali na lenye kufanya mapenzi yake? Ninajikaza sana kuhubiri na kufundisha watu habari njema ya Ufalme? Matendo yangu yanaonyesha kama ninaamini kabisa kwamba hizi ni siku za mwisho na kama mwisho wa utawala wa Shetani unakaribia? Ninaendelea kutumainia kabisa Yehova na Yesu kama vile nilikuwa ninawatumainia wakati nilitoa maisha yangu kwa Yehova Mungu?’ (Mt. 24:14; 2 Tim. 3:1; Ebr. 3:14) Kufikiri sana juu ya majibu ya maulizo hayo kutatusaidia kujua ikiwa tuko watu wa namna gani.

6. (a) Ni njia gani moja tu yenye kuongoza kwenye uzima? (b) Namna gani muzee mumoja anajitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho wa kila mwaka, na namna gani wewe pia unaweza kufanya hivyo?

6 Soma na ufikiri sana juu ya habari zenye kutegemea Maandiko zenye kufasiria sababu gani tukio hilo ni la maana sana. (Soma Yohana 3:16; 17:3.) Njia moja tu yenye kuongoza kwenye uzima wa milele ni “kupata ujuzi” juu ya Yehova na ‘kumuamini’ Yesu, Mwana wake wa pekee. Ili kujitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho, unaweza kuchagua habari fulani za kujifunza zenye zitakusaidia kumukaribia zaidi Yehova na Yesu. Fikiria mambo yenye ndugu mumoja mwenye amekuwa muzee wa kutaniko kwa miaka mingi anazoea kufanya. Kwa miaka mingi, amekusanya habari za Munara wa Mulinzi zenye kuzungumuzia sana Ukumbusho na upendo wenye Yehova na Yesu wametuonyesha. Katika majuma fulani mbele ya Ukumbusho, anasoma tena habari hizo na kufikiri sana juu ya faida za tukio hilo. Wakati fulani, anaongezea kwenye habari hizo habari moja ao mbili za mupya. Muzee huyo ametambua kama kwa kusoma tena habari hizo na kusoma na kufikiri sana juu ya usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho, anajifunza mambo ya mupya kila mwaka. Jambo la maana zaidi, anajisikia kama upendo wake kwa Yehova na Yesu unaongezeka kila mwaka. Mupango huo wa kujifunza unaweza kukusaidia wewe pia kukomalisha upendo wako na shukrani yako kwa Yehova na Yesu, na hilo linaweza kukusaidia ufaidike kabisa na Ukumbusho.

UKUMBUSHO UNATIA NGUVU UMOJA WETU

7. (a) Yesu alisali juu ya nini katika usiku wa Chakula cha kwanza cha Bwana cha Mangaribi? (b) Ni nini inaonyesha kuwa Yehova amejibia sala ya Yesu?

7 Katika usiku wa Chakula cha kwanza cha Bwana cha Mangaribi, Yesu alisali kwamba wanafunzi wake wote waungane na wakuwe na umoja kama ule wenye yeye na Baba yake wanafurahia sana. (Soma Yohana 17:20, 21.) Kwa kweli, Yehova amejibia sala hiyo ya Mwana wake mupendwa, na sasa mamilioni ya watu wanaamini kama Yehova alituma Mwana wake. Kuliko mukutano mwingine wowote wa watu wa Mungu, Ukumbusho unaonyesha wazi kabisa umoja wa Mashahidi wa Yehova. Watu wa mataifa mengi na wa rangi mbalimbali ya ngozi wanakusanyika pamoja mahali mbalimbali katika dunia yote. Katika maeneo fulani haiko jambo la kawaida watu wa rangi mbalimbali ya ngozi kukusanyika pamoja kwa ajili ya mambo ya dini, ao ikiwa wanafanya hivyo, watu wengine wanaona kuwa jambo hilo halifae. Lakini Yehova na Yesu wanafurahia umoja huo!

8. Ni ujumbe gani wenye Yehova alimupatia Ezekieli juu ya umoja?

8 Kwa sababu sisi ni watu wa Yehova, umoja wenye tuko nao hautushangaze. Kwa kweli, Yehova alitabiri jambo hilo. Fikiria ujumbe wenye alimupatia nabii Ezekieli juu ya kuunganisha vijiti ao vipande viwili vya muti, kijiti “kwa Yuda” na kijiti “kwa Yosefu.” (Soma Ezekieli 37:15-17.) Habari yenye kichwa, “Maulizo ya Wasomaji Wetu,” yenye ilichapishwa katika Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 7, 2016, ilieleza hivi: “Kupitia nabii wake Ezekieli, Yehova alitabiri kama watu wake wangerudia katika Inchi ya Ahadi na kama wangeungana na kuwa tena taifa moja. Unabii huo ulitabiri pia kama wale wenye kumuabudu Mungu katika siku za mwisho wangeungana na kuwa taifa moja.”

9. Namna gani utimizo wa unabii wa Ezekieli unaonekana kila mwaka kwenye Ukumbusho?

9 Kuanzia mwaka wa 1919 na kuendelea, kwanza Yehova alipanga tena na kuunganisha tena pamoja watiwa-mafuta hatua kwa hatua, wenye walifananishwa na kijiti “kwa Yuda.” Kisha, wakati watu wengi zaidi wale wenye kuwa na tumaini la kuishi duniani wenye kufananishwa na kijiti “kwa Yosefu,” waliendelea kujiunga na watiwa-mafuta, vikundi hivyo viwili vikakuwa “kundi moja.” (Yoh. 10:16; Zek. 8:23) Yehova aliahidi kuunganisha vijiti hivyo viwili na kuvifanya kuwa kimoja katika mikono yake. (Eze. 37:19) Leo vikundi hivyo viwili vinatumika katika umoja chini ya uongozi wa Mufalme mumoja, ni kusema, Yesu Kristo mwenye ametukuzwa, mwenye unabii unazungumuzia kuwa ‘Daudi mutumishi’ wa Mungu. (Eze. 37:24, 25) Umoja huo wa maana wenye kuzungumuziwa katika Ezekieli unaonekana wazi kila mwaka wakati watiwa-mafuta wenye wangali duniani na “kondoo wengine” wanakusanyika pamoja ili kufanya Ukumbusho wa kifo cha Kristo! Lakini, kila mumoja wetu anaweza kufanya nini ili kulinda na kuendeleza umoja huo?

NAMNA KILA MUMOJA WETU ANAWEZA KUENDELEZA UMOJA

10. Namna gani tunaweza kuendeleza umoja kati ya watu wa Mungu?

10 Njia moja yenye tunaweza kutumia ili kuendeleza umoja wa watu wa Mungu ni kuonyesha sifa ya unyenyekevu. Wakati alikuwa duniani, Yesu alishauria wanafunzi wake wakuwe wanyenyekevu. (Mt. 23:12) Ikiwa tuko wanyenyekevu, hatutaambukizwa na roho ya watu wa ulimwengu ya kujipandisha. Lakini, unyenyekevu wetu utatusaidia kujitiisha kwa wale wenye kuongoza, na roho kama hiyo ya utii ni ya maana sana ili kuendeleza umoja katika kutaniko. Jambo la maana zaidi ni kwamba, unyenyekevu wetu unamupendeza Mungu, kwa sababu ‘anawapinga wenye majivuno, lakini anawapatia wanyenyekevu fazili zisizostahiliwa.’​—1 Pet. 5:5.

11. Namna gani kufikiri juu ya maana ya mukate na divai vyenye kutumiwa kwenye Ukumbusho kunatusaidia kuendeleza umoja?

11 Njia ya pili yenye tunaweza kutumia ili kuendeleza umoja ni kufikiri sana juu ya mukate na divai vyenye kutumiwa kwenye Ukumbusho. Mbele ya usiku huo wa pekee, na zaidi sana wakati wa usiku huo, ufikiri sana juu ya maana ya mukate huo wenye hauna chachu na divai nyekundu. (1 Kor. 11:23-25) Mukate unafananisha mwili wa Yesu wenye hauna zambi wenye ulitolewa kama zabihu, na divai inafananisha damu yake yenye alimwanga. Lakini tunapaswa kufanya mengi zaidi kuliko kuelewa tu maana ya mukate na divai. Kumbuka kama zabihu ya ukombozi ya Kristo inatia ndani matendo mawili makubwa zaidi yenye kuonyesha upendo; kwanza upendo wenye Yehova alionyesha kwa kutoa Mwana wake kwa ajili yetu, na pili upendo wenye Yesu alionyesha kwa kuwa tayari kutoa uzima wake kwa ajili yetu. Kufikiri sana juu ya upendo wao kunapaswa kutuchochea tuwapende pia. Na upendo wenye sisi wote tuko nao kwa Yehova uko kama kamba yenye kutuunganisha pamoja na unatia nguvu umoja wetu.

Wakati tunasamehe wengine, tunaendeleza umoja (Picha hizi zinapatana na fungu la 12, 13)

12. Katika mufano wa mufalme na watumwa wake, namna gani Yesu alionyesha wazi kama Yehova anapenda tukuwe wenye kusamehe wengine?

12 Njia ya tatu yenye tunaweza kutumia ili kuendeleza umoja ni kuwa tayari kusamehe wengine. Wakati tunasamehe wale wenye walitukosea, tunaonyesha kama tunapendezwa na musamaha wa zambi zetu wenye tulipata kupitia zabihu ya ukombozi ya Kristo. Fikiria mufano mumoja wa Yesu wenye kupatikana katika Mathayo 18:23-34. Ujiulize hivi: ‘Niko tayari kutumikisha mambo yenye Yesu alifundisha? Ninaonyesha uvumilivu watumishi wenzangu na kuwaelewa? Niko tayari kusamehe wale wenye wananikosea?’ Ni kweli kwamba, zambi zinatofautiana, na wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kuona kuwa ni vigumu kusamehe makosa fulani. Lakini, mufano huu unatufundisha mambo yenye Yehova anapenda tufanye. (Soma Mathayo 18:35.) Yesu anaonyesha wazi kama Yehova hatatusamehe ikiwa hatusamehe ndugu ao dada zetu wakati wanatubu kwelikweli. Tunapaswa kufikiria sana jambo hilo! Tunaendeleza na kuulinda umoja wetu wa maana sana wakati tunasamehe wengine kama vile Yesu alitufundisha.

13. Namna gani kuwa watu wenye kufanya amani kunaendeleza umoja?

13 Wakati tunasamehe wengine, tunaonyesha wazi kama tuko watu wenye kufanya amani. Kumbuka shauri la mutume Paulo lenye kuonyesha kama tunapaswa ‘kujitahidi [ao, kujikaza] sana kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.’ (Efe. 4:3) Katika kipindi cha Ukumbusho na zaidi sana usiku wa Ukumbusho, ufikiri sana juu ya namna unatendea wengine. Ujiulize hivi: ‘Ninajulikana kuwa mutu mwenye kuepuka kuweka kinyongo? Ninajulikana kuwa mutu mwenye kuwa tayari kufuatia amani na umoja?’ Ni muzuri kufikiria sana maulizo hayo mazito katika kipindi hiki cha mwaka.

14. Namna gani tunaweza kuonyesha kama ‘tunavumiliana katika upendo’?

14 Njia ya ine yenye tunaweza kutumia ili kuendeleza umoja ni kuonyesha upendo kwa kumuiga Yehova, Mungu mwenye upendo. (1 Yoh. 4:8) Usiseme hata kidogo juu ya ndugu na dada zako kuwa, “Ninaweza kuwapenda kwa sababu ni ndugu zangu, lakini kwa kweli, silazimike kuwafurahia”! Mawazo hayo hayapatane na shauri la mutume Paulo lenye kusema kwamba tunapaswa ‘kuvumiliana katika upendo.’ (Efe. 4:2) Ona kwamba hakusema tu kama tunapaswa ‘kuvumiliana.’ Aliongeza kama tunapaswa kufanya hivyo “katika upendo.” Kuko tofauti. Katika makutaniko yetu kuko watu wa namna zote wenye Yehova amevuta kwake. (Yoh. 6:44) Kwa sababu Yehova amewavuta kwake, aliona kuwa wanastahili kupendwa. Kwa hiyo, hakuna mumoja kati yetu anaweza kusema kama ndugu ao dada fulani hastahili kuonyeshwa upendo. Hatupaswe kujizuia kuonyesha upendo wenye Yehova anatuomba tuonyeshe!​—1 Yoh. 4:20, 21.

UKUMBUSHO WA MWISHO UTAFANYWA WAKATI GANI?

15. Namna gani tunajua kama kutakuwa Ukumbusho wa mwisho?

15 Siku moja, Ukumbusho utafanywa kwa mara ya mwisho. Tunajua hilo namna gani? Katika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho yenye kuongozwa na roho ya Mungu, Paulo aliandikia Wakristo watiwa-mafuta kama kwa kukumbuka kifo cha Yesu kila mwaka, ‘wanaendelea kukitangaza kifo cha Bwana, mupaka atakapofika.’ (1 Kor. 11:26) Neno “kufika” linazungumuzia tukio lilelile la “kuja” lenye Yesu alizungumuzia katika unabii wake juu ya wakati wa mwisho. Juu ya ziki kubwa yenye kuwa mbele yetu, alisema hivi: ‘Ndipo ishara ya Mwana wa binadamu itakapoonekana mbinguni, ndipo makabila yote ya dunia yatakapojipiga-piga yenyewe kwa kuomboleza, nayo yatamuona Mwana wa binadamu akija juu ya mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mwingi. Naye [Yesu] atawatuma malaika zake pamoja na muvumo [ao, sauti] mukubwa wa tarumbeta, nao watawakusanya pamoja watu wake waliochaguliwa kutoka kwenye zile pepo ine, kutoka mwisho mumoja wa mbingu mupaka mwisho wake mwingine.’ (Mt. 24:29-31) Tukio la ‘kukusanya pamoja watu wake waliochaguliwa’ linazungumuzia wakati Wakristo watiwa-mafuta wote wenye wangali duniani watapata zawadi yao ya kuenda mbinguni. Hilo litafanyika kisha sehemu ya kwanza ya ziki kubwa kumalizika, lakini mbele ya vita ya Har-magedoni kuanza. Kisha wale wote 144000 watajiunga na Yesu ili kupata ushindi juu ya wafalme wa dunia. (Ufu. 17:12-14) Ukumbusho wenye utafanywa mbele ya kukusanywa kwa watiwa-mafuta hao ili kuenda mbinguni, utakuwa wa mwisho kwa sababu Yesu atakuwa ‘amefika.’

16. Sababu gani utajikaza sana ili ukuwe kwenye Ukumbusho wa mwaka huu?

16 Tuazimie basi kupata faida kwa kuhuzuria Ukumbusho wa tarehe 31 Mwezi wa 3, 2018. Na tumuombe Yehova atusaidie tuendeleze umoja kati ya watu wake! (Soma Zaburi 133:1.) Ukumbuke kama siku moja tutafanya Ukumbusho wa mwisho. Mbele siku hiyo ifike, tujikaze basi kuhuzuria, na tupendezwe na umoja wenye tunafurahia wakati wa Ukumbusho.