Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 12

Unawezaje Kuwa na Familia Yenye Furaha?

Unawezaje Kuwa na Familia Yenye Furaha?

Upendo ndio siri ya kuwa na furaha katika familia. Waefeso 5:33

Kulingana na sheria ya Mungu, ndoa inapaswa kuwa kati ya mwanamume mmoja na mwanamke mmoja.

Mume mwenye upendo anamtendea mke wake kwa wororo na uelewaji.

Mke anapaswa kushirikiana na mume wake.

Watoto wanapaswa kuwatii wazazi wao.

Uwe mwenye fadhili na mwaminifu, usiwe mkatili au kukosa uaminifu. Wakolosai 3:5, 8-10

Neno la Mungu linasema kwamba mume anapaswa kumpenda mke wake kama mwili wake mwenyewe na kwamba mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.

Ni kosa kufanya ngono nje ya ndoa. Ni kosa pia kuoa wake wengi.

Neno la Yehova linafundisha familia jinsi zinavyoweza kuwa na furaha.