WIMBO NA. 53
Kujitayarisha Kuhubiri
-
1. Mapema,
Asubuhi,
Siku ya kuhubiri.
Kungali giza,
Na mvua yaanza.
Twatamani kuendelea
Kulala.
(KORASI)
Tutafanikiwa kwa sala,
Na matayarisho;
Nao mtazamo mzuri,
Twahitaji.
Malaika wanaongoza.
Yesu wamtii.
Bega kwa bega na wenzetu,
Hatushindwi.
-
2. Furaha,
Tutapata
Tukikumbuka hili:
Bidii yetu,
Yehova aona.
Upendo wetu akumbuka,
Twajua.
(KORASI)
Tutafanikiwa kwa sala,
Na matayarisho;
Nao mtazamo mzuri,
Twahitaji.
Malaika wanaongoza.
Yesu wamtii.
Bega kwa bega na wenzetu,
Hatushindwi.
(Ona pia Mhu. 11:4; Mt. 10:5, 7; Luka 10:1; Tito 2:14)