Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 5

Kazi za Mungu za Ajabu

Kazi za Mungu za Ajabu

(Zaburi 139)

  1. 1. Mungu, wanijua vizuri,

    Nilalapo na niamkapo.

    Na fikira zangu umechunguza,

    Maneno na matendo yangu

    wajua.

    Sirini nilipofanyizwa,

    Uliiona mifupa yangu.

    Yote yalikuwa yameandikwa.

    Unastahili sifa

    na utukufu.

    Ee, Yehova, una hekima nyingi;

    Nafsi yangu inajua vema.

    Hata katika giza la usiku,

    Roho yako itaniongoza.

    Yehova nijifiche wapi,

    Kutoka mbele za uso wako?

    Si Kaburini wala si mbinguni,

    Gizani wala baharini,

    siwezi.