WIMBO NA. 5
Kazi za Mungu za Ajabu
-
1. Mungu, wanijua vizuri,
Nilalapo na niamkapo.
Na fikira zangu umechunguza,
Maneno na matendo yangu
wajua.
Sirini nilipofanyizwa,
Uliiona mifupa yangu.
Yote yalikuwa yameandikwa.
Unastahili sifa
na utukufu.
Ee, Yehova, una hekima nyingi;
Nafsi yangu inajua vema.
Hata katika giza la usiku,
Roho yako itaniongoza.
Yehova nijifiche wapi,
Kutoka mbele za uso wako?
Si Kaburini wala si mbinguni,
Gizani wala baharini,
siwezi.
(Ona pia Zab. 66:3; 94:19; Yer. 17:10.)