Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 20

Ulitoa Mwana Wako Mpendwa

Ulitoa Mwana Wako Mpendwa

(1 Yohana 4:9)

  1. 1. Yehova, Ee Baba,

    Tu watenda-dhambi

    Fidia imetupa

    tumaini!

    Twataka kufanya

    yote tuwezayo

    Wengine wajue,

    wema wako wote.

    (KORASI)

    Mwanao mpendwa,

    Ulitoa afe.

    Tutaimba milele,

    Kwa kutupa Mwana wako.

  2. 2. Fadhili, rehema,

    Zatuvuta kwako.

    Twasema asante,

    na twathamini

    kutoa Mwanao

    kwa ajili yetu

    uzima tupate

    twashukuru sana.

    (KORASI)

    Mwanao mpendwa,

    Ulitoa afe.

    Tutaimba milele,

    Kwa kutupa Mwana wako.

    (UMALIZIO)

    Yehova, Ee Baba, Tunakushukuru.

    Twasema asante, kutoa Mwana wako.

(Ona pia Yoh. 3:16; 15:13.)