WIMBO NA. 123
Kutii Utaratibu wa Kitheokrasi kwa Ushikamanifu
-
1. Watu wa Yehova tutangazapo,
Kweli za Ufalme zenye thamani.
Utaratibu wa kitheokrasi,
Lazima tutii, kuwe umoja.
(KORASI)
Tuna wajibu wa kumtii
Yehova milele.
Anatupenda, na kutulinda.
Twashikamana naye.
-
2. Mungu ametupa mtumwa wake,
Pia roho yake ituongoze.
Na twende sambamba; bega kwa bega,
Tujulishe wote amri za Mungu.
(KORASI)
Tuna wajibu wa kumtii
Yehova milele.
Anatupenda, na kutulinda.
Twashikamana naye.
(Ona pia Luka 12:42; Ebr. 13:7, 17.)