Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Watu Watafuta Majibu

Watu Watafuta Majibu

Watu Watafuta Majibu

“Karibu kila mtu ana maoni fulani kumhusu [Yesu].” Iwe tunamwamini Yesu au la, sisi sote hujiuliza swali hili: ‘Mtu huyu ni nani?’”​—MWANDISHI STAN GUTHRIE.

WATU wanataka kujua mambo mengi kumhusu Yesu. Sinema na vitabu vinavyomhusu vinapendwa sana. Hata hivyo, watu wengi bado wana maswali kumhusu Yesu, na maoni yao yanatofautiana sana.

Miaka michache iliyopita, waandishi wa habari waliwaomba watu wajibu swali hili kwenye mtandao wa Intaneti: “Yesu ni nani?” Yafuatayo ni baadhi ya majibu waliyopata:

● “Yaelekea alikuwa rabi (mwalimu) mwenye huruma sana.”

● “Alikuwa mtu wa kawaida aliyeishi maisha yasiyo ya kawaida.”

● “Hakuna uthibitisho wowote kwamba mtu aliyeitwa Yesu alikuwapo.”

● “Yesu ni Mwana wa Mungu ambaye alizaliwa, akafa, na kufufuliwa ili atuokoe kutoka kwa dhambi zetu. Yeye yuko hai, na atakuja duniani tena.”

● “Ninaamini Yesu Kristo ni mwana pekee wa Mungu, yeye ni mwanadamu, na wakati uleule yeye ni Mungu.”

● “Ni watoto tu wanaoweza kuamini hadithi kumhusu Yesu.”

Ni wazi kwamba maoni hayo yote yanayotofautiana sana, hayawezi kuwa sahihi. Je, kuna chanzo chochote cha habari kinachoweza kutupa majibu yaliyo sahihi kumhusu Yesu? Wachapishaji wa gazeti hili wanaamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu na ndicho kitabu pekee kinachotuambia ukweli kumhusu Yesu. *2 Timotheo 3:16.

Katika makala inayofuata, tutachunguza majibu ya Biblia ya maswali ambayo watu wengi huuliza kumhusu Yesu. Yeye mwenyewe alisema “kila mtu anayemwamini” atapata wokovu. (Yohana 3:16) Tunakuomba uchunguze majibu hayo ili uamue mwenyewe kama utahitaji kujifunza mengi zaidi kumhusu Yesu na jinsi unavyoweza kuonyesha kwamba unamwamini.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 11 Ili kupata habari zaidi, ona sura ya 2 yenye kichwa “Biblia​—Kitabu Kutoka kwa Mungu,” katika kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.