Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mwanamume na Mwanamke Wameumbwa Ili Wakamilishane

Mwanamume na Mwanamke Wameumbwa Ili Wakamilishane

Mwanamume na Mwanamke Wameumbwa Ili Wakamilishane

MWANAMUME na mwanamke wanatamani sikuzote kuwa pamoja. Mungu ndiye aliyewaumba wakiwa na tamaa hiyo. Yehova aliona kwamba si vema mwanamume wa kwanza Adamu aendelee kuwa peke yake. Kwa hiyo, Mungu akamfanyia “msaidizi, awe kikamilisho chake.”

Yehova alimletea Adamu usingizi mzito, kisha akachukua ubavu wake mmoja na ‘kuufanya ubavu huo kuwa mwanamke na kumleta kwa huyo mwanamume.’ Adamu alisisimka sana alipokutana na kiumbe huyo mrembo aliyeumbwa na Yehova hivi kwamba akasema: “Mwishowe huyu ni mfupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu.” Kwa kweli, mwanamke mkamilifu Hawa, alikuwa mwenye kupendeka sana kwa sababu ya sifa zake za kike. Naye Adamu mkamilifu alistahili kuheshimiwa kwa sababu ya sifa zake za kiume. Waliumbwa ili wakamilishane. Biblia inasema hivi: “Hiyo ndiyo sababu mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake nao watakuwa mwili mmoja.”—Mwanzo 2:18-24.

Hata hivyo, familia zinavunjika leo na mara nyingi wanaume na wanawake wanatendeana vibaya au wanaongozwa na uchoyo. Roho ya mashindano kati ya wanaume na wanawake imesababisha mvurugo na kutopatana. Yote hayo hayapatani na kusudi la Mungu kwa ajili ya mwanamume na mwanamke. Mwanamume aliumbwa ili atimize wajibu wa maana duniani. Mwanamke alikusudiwa awe na wajibu wa pekee na wenye heshima akiwa kikamilisho cha mwanamume. Walipaswa kufanya kazi pamoja kwa upatano. Tangu wanadamu walipoumbwa, wanaume na wanawake wanaomwogopa Mungu wamejitahidi kutimiza kwa uaminifu wajibu ambao Yehova aliwapa, na hilo limewafanya wawe wenye furaha na wenye kuridhika zaidi. Ni wajibu gani huo, na tunaweza kuutimiza jinsi gani?

[Picha katika ukurasa wa 3]

Mwanamume na mwanamke waliumbwa ili watimize wajibu wenye kuheshimika katika mpango wa Mungu