Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mungu Anahisije Anapoona Ukiteseka?

Mungu Anahisije Anapoona Ukiteseka?

Baadhi ya watu wanaamini kwamba Mungu haoni mateso wanayokabili na wala hajali.

FIKIRIA KILE AMBACHO BIBLIA INASEMA

  • Mungu anaona na anajali

    “Yehova akaona kwamba uovu wa mwanadamu ulikuwa mkubwa duniani . . . , na moyo wake ukahuzunika.”—Mwanzo 6:5, 6.

  • Mungu atakomesha mateso yote

    “Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawatakuwepo tena; utapaangalia mahali walipokuwa, nao hawatakuwepo. Lakini wapole wataimiliki dunia, nao watafurahia kwelikweli wingi wa amani.” —Zaburi 37:10, 11.

  • Mipango ya Mungu kwa ajili yako

    “‘Ninajua vizuri mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi,’ asema Yehova, ‘mawazo ya amani, wala si ya msiba, ili niwape ninyi wakati ujao na tumaini. Nanyi mtaniita na kuja na kusali kwangu, nami nitawasikiliza.’”—Yeremia 29:11, 12.

    “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”—Yakobo 4:8.