Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Uko Tayari Kuhudhuria?

Je, Uko Tayari Kuhudhuria?

Je, Uko Tayari Kuhudhuria?

▪Je, uko tayari kuhudhuria Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova la “Utii wa Kimungu”? Mfululizo huo wa makusanyiko ya siku tatu, yaliyoanza nchini Marekani juma la mwisho la Mei, umepangiwa kufanywa katika miezi kadhaa ijayo kwenye majiji mengi ulimwenguni kote. Bila shaka moja litafanyiwa katika jiji lililo karibu nawe.

Katika sehemu nyingi, kusanyiko litaanza saa 3:30 asubuhi kwa programu ya muziki. Kichwa cha Ijumaa ni “Tiini Sauti Yangu, Nami Nitakuwa Mungu Wenu.” (Yeremia 7:23) Baada ya hotuba za asubuhi zenye kichwa “Tumeumbwa kwa ‘Njia ya Ajabu’” na “Kwa Nini Tumaini la Ufufuo Lapaswa Kuwa Halisi Kwako,” kipindi kitamalizika kwa hotuba ya msingi, “Fuateni Kielelezo Mlichowekewa Katika Kumtii Mungu.”

Kipindi cha Ijumaa alasiri kitakuwa na hotuba “Endeleeni ‘Kukaza Akili Juu ya Roho,’ Mpate Uzima,” “Jilindeni na Kila Namna ya Tamaa,” na “Usifuate ‘Hadithi za Uwongo Zilizotungwa kwa Ufundi.’” Kisha kutakuwa na mfululizo wenye sehemu mbili utakaozungumzia mambo makuu ya vitabu vya Biblia vya Hagai na Zekaria. Siku ya kwanza itamalizika kwa hotuba “Kila Namna ya Kuteseka Itakwisha Karibuni!”

Kichwa cha programu ya Jumamosi ni ‘Utii Kutoka Moyoni’ “Katika Mambo Yote,” kinategemezwa na Waroma 6:17 na 2 Wakorintho 2:9. Kipindi cha asubuhi kitatia ndani mfululizo wenye sehemu tatu wenye kichwa “Familia Zinazotii Kanuni za Mungu Hupata Furaha.” Mfululizo huo utakuwa na maonyesho na mahoji na utakazia jinsi washiriki wa familia—mume, mke, na watoto—wanavyoweza kuchangia furaha ya familia. Programu ya asubuhi itamalizika kwa sehemu yenye kichwa “Acheni Ndiyo Yenu Imaanishe Ndiyo,” na baada ya hapo wale wanaostahili watabatizwa.

Hotuba za Jumamosi alasiri zitatia ndani, “Usione Mambo Yasiyofaa” na “Rudini kwa Mchungaji wa Nafsi Zenu.” Mfululizo wenye sehemu mbili wenye kichwa, “Watiini Wale Wanaoongoza” utafuata. Hotuba ya mwisho alasiri hiyo yenye kichwa, “Biblia Inafundisha Nini Hasa?” ni hotuba muhimu ya kusanyiko.

Programu ya Jumapili asubuhi itazungumzia kichwa “Utii Maneno Yote Haya . . . Ili Mambo Yakuendee Vema,” kikitegemezwa na Kumbukumbu la Torati 12:28. Mfululizo wenye sehemu tatu wenye kichwa “Wasaidie Wengine Watii Mambo Ambayo Biblia Inafundisha” utatoa msaada wenye kutumika katika kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo.

Kipindi cha asubuhi kitamalizika kwa drama ya nyakati za Biblia yenye kichwa “Fuatia Miradi Inayomletea Mungu Heshima.” Itatanguliwa na hotuba yenye kichwa “Vijana—Je, Miradi Yenu Itawawezesha Kufanikiwa?” Hotuba hiyo itaeleza juu ya drama ya Biblia itakayofuata ambayo inahusu kijana Timotheo, aliyeweka mfano wa kujitoa bila ubinafsi ambao vijana leo wanatiwa moyo waige. Kipindi cha mwisho cha kusanyiko Jumapili alasiri kitakuwa na hotuba ya watu wote yenye kichwa, “Ni Nani Tunayemtii?”

Fanya mipango sasa ili uhudhurie. Ili kujua mahali ambapo kusanyiko la kwenu litafanywa, tembelea Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova au waandikie wachapishaji wa gazeti hili. Katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, kuna orodha ya mahali ambapo makusanyiko yote yatafanywa nchini Burundi, Kenya, Kongo (Kinshasa), Rwanda, Tanzania, na Uganda.