Kutoka kwa Wasomaji Wetu
Kutoka kwa Wasomaji Wetu
Kudhulumiwa Kazini Nilipendezwa sana na mfululizo uliokuwa na kichwa “Ufanyeje Ukidhulumiwa Kazini?” (Mei 8, 2004) Mambo yote yaliyotajwa katika makala hiyo yamenipata. Nilibaguliwa kwa sababu ya dini yangu katika hospitali ambayo nilifanya kazi, na jambo hilo liliniathiri kihisia na kiroho. Ninafurahi kujua kwamba si mimi peke yangu nimekabili hali ngumu jinsi hiyo.
J. C., Puerto Riko
Nilidhulumiwa kwa miaka kadhaa na nilikuwa karibu kupatwa na matatizo ya akili na ya kihisia. Nitajitahidi sana kutumia mapendekezo yenu.
C. H., Marekani
Asanteni kwa kutusaidia sisi tunaodhulumiwa na kutusaidia kumkaribia Mungu wetu mwenye huruma, ambaye anatambua kwamba tunateseka.
L. W., Marekani
Kutaniko letu la Mashahidi wa Yehova lilitoa gazeti hili katika maeneo ya kazi na kuwatia moyo waajiri waiweke makala hiyo katika faili. Watu wengi walishukuru sana kwa habari hiyo.
V. S., Marekani
Nililazimika kuacha kazi kwa sababu ya kutukanwa. Tafadhali endeleeni kuchapisha makala zinazotuonyesha jinsi ya kukabiliana na matatizo.
T. Y., Japani
Nilimpa daktari wangu gazeti hilo na kumwambia, “Labda siku moja mgonjwa anayeumwa na tumbo atakuja kukuona kwa sababu ya kudhulumiwa kazini.” Aliniambia, “Usiseme labda kwa sababu sasa hivi nina mgonjwa anayekabili hali hiyo!” Daktari huyo alisema atasoma makala hizo.
E. S., Ujerumani
Kwa kuwa sina makao, inanibidi kuishi na dada yangu na kuvumilia matusi yake. Jambo hilo limenifanya nishuke moyo sana. Hata hivyo, gazeti hilo la Amkeni! lilinifaa kabisa! Kwa kweli Yehova amenifariji.
S. A., Urusi
Mimea Inayoua Asanteni sana kwa makala yenye kichwa “Jihadhari na Mimea Inayoua.” (Mei 8, 2004) Nimekuwa nikikusanya na kutunza mimea inayokula wadudu kwa zaidi ya miaka 12. Makala hiyo ilizungumzia mambo ya kisayansi kwa usahihi kabisa na kwa njia rahisi.
T. K., Ujerumani
Nina umri wa miaka 11 na mwalimu wetu alituagiza tuandike kuhusu mmea wa kinasa-nzi. Makala hiyo ilikuja juma hilohilo, kwa wakati unaofaa kabisa.
R. S., Urusi
Nilikuwa nikikuza mimea inayokula wadudu na makala hiyo ilinipendeza sana. Lakini sikubaliani kabisa na kichwa cha makala hiyo. Ingawa mimea hiyo inaweza kuhatarisha wadudu fulani, hiyo ni mimea safi na inaweza kuharibika kwa urahisi. Mimea fulani kama hiyo imo hatarini.
H. K., Japani
“Amkeni!” linajibu: Asante kwa kikumbusha hicho. Ingawa kichwa cha makala hiyo kilitumiwa kuwavuta wasomaji, makala yenyewe iliwafundisha wasomaji kwamba wanapaswa kuheshimu na kutunza mimea hiyo.
Imani Yajaribiwa Nilifurahia makala yenye kichwa “Imani ya Familia Yajaribiwa.” (Mei 8, 2004) Nina umri wa miaka kumi na nina ugonjwa wa Crohn. Nililazwa hospitali mara nyingi sana katika majira yaliyopita ya baridi kali hadi ugonjwa wangu ulipogunduliwa. Makala hiyo ilinisaidia niwe na ujasiri zaidi na niweze kukabiliana na ugonjwa wangu. Ninatazamia kwa hamu kuishi katika Paradiso, wakati ambapo hatutapatwa na matatizo hayo tena.
M. H., Marekani