Jinsi Unavyoweza Kumkaribia Mungu

Jinsi Unavyoweza Kumkaribia Mungu

Jinsi Unavyoweza Kumkaribia Mungu

Wengi wamependekeza watu wasome kitabu Mkaribie Yehova. Mtu mmoja aliyesoma kitabu hicho aliandika hivi: “Nimemaliza tu kukisoma, nami sijawahi kuchochewa jinsi hiyo. Asanteni sana kwa kunikumbusha kwa njia mbalimbali kwamba Yehova ni Baba mwenye upendo, anayejali, na mwenye fadhili.”

Mwingine alieleza hivi kuhusu jinsi alivyohisi: “Kitabu hicho kimenisaidia kumjua zaidi Baba yangu, kuyafahamu mawazo yake ya ajabu, na upendo mwingi alio nao kwa kila mmoja wetu. Kusoma kitabu hicho ni kama kushika almasi maridadi inayong’aa, iliyo na thamani kubwa, kisha kuigeuza polepole huku ukiichunguza kwa makini, kwani kila sura mpya hupendeza zaidi na zaidi.”

Pia mwanamke fulani alisema hivi: “Nimemaliza tu kusoma kitabu Mkaribie Yehova. Nilipokuwa nikisoma mafungu mawili ya mwisho ya kitabu hicho, ilinibidi kutua ili nisali, kwa kuwa nilistaajabu na kujawa na upendo. Sasa ninampenda na kumthamini Yehova zaidi.”

Tunasadiki kwamba wewe pia utahisi vivyo hivyo ikiwa utakisoma kitabu hicho chenye kurasa 320. Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Mkaribie Yehova bila malipo. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.