MAISHA YA MKRISTO

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuhubiri Kupitia Simu

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuhubiri Kupitia Simu

KWA NINI NI MUHIMU: Kuhubiri kupitia simu ni njia muhimu ya “kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema.” (Mdo 20:24) * Inatuwezesha kumtolea mtu ushahidi wakati ambapo hali hazituruhusu kumtembelea.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Tayarisha. Chagua habari inayofaa. Kisha tayarisha muhtasari wa kile unachotaka kusema. Ni muhimu kuketi mezani ukiwa na muhtasari na vitu vingine vyote utakavyohitaji, kama vile kifaa cha kielektroni kilichofunguliwa programu ya JW Library® au jw.org®

  • Tulia. Zungumza kwa njia ya kawaida. Tabasamu na utoe ishara kana kwamba mtu unayezungumza naye anakuona. Epuka kutua-tua bila sababu. Inafaa kuhubiri pamoja na wengine. Mwenye-nyumba anapouliza swali, rudia swali hilo kwa sauti ili mwandamani wako akusaidie kutafuta jibu

  • Weka msingi wa ziara ya kurudia. Mtu akionyesha upendezi, unaweza kumwachia swali utakalojibu unapompigia simu tena. Unaweza pia kumwomba umpelekee chapisho letu au umtumie kupitia barua-pepe au barua. Au unaweza kumtumia video au makala kupitia ujumbe au barua-pepe. Inapofaa, mwambie kuhusu jambo fulani kwenye tovuti yetu

^ fu. 3 Ikiwa katika eneo lenu inaruhusiwa kuhubiri kupitia simu, unapaswa kufuata sheria zinazofaa za kushughulikia habari za mtu mwingine.