Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | YOHANA 20-21

“Je, Unanipenda Kuliko Hawa?”

“Je, Unanipenda Kuliko Hawa?”

21:1-19

Katika nyakati za Biblia, wavuvi waliofanikiwa walikuwa wenye subira, walifanya kazi kwa bidii, na walikuwa tayari kuvumilia hali ngumu ili waweze kupata samaki. (w12 8/1 18-20) Sifa hizo zingemsaidia Petro awe mvuvi mzuri wa watu. Hata hivyo, Petro alihitaji kuamua ni kipi cha kutangulizwa maishani mwake—kazi ya kimwili aliyofurahia au kazi ya kuwalisha kiroho wafuasi wa Yesu.

Ni marekebisho gani ambayo umefanya ili uweze kutanguliza masilahi ya Ufalme?