Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Jinsi ya Kutumia JW Library

Jinsi ya Kutumia JW Library

UNAPOJIFUNZA:

  • Soma Biblia na andiko la siku

  • Soma Kitabu cha Mwaka, magazeti, na machapisho mengine. Tia alama ukurasa ili ukumbuke ulipofikia

  • Tayarisha mikutano ya kutaniko, na upige mistari kwenye majibu

  • Tazama video

KATIKA MIKUTANO:

  • Soma maandiko yanayotajwa na msemaji. Tumia historia ili kurudi kwenye maandiko uliyokuwa umefungua

  • Badala ya kubeba machapisho mengi kwenye mkutano, tumia kifaa chako wakati wa sehemu za mkutano na mnapoimba. Programu ya JW Library ina nyimbo mpya ambazo hazipatikani katika kitabu cha nyimbo

KATIKA HUDUMA:

  • Mwonyeshe mtu anayependezwa jambo fulani katika JW Library, kisha umsaidie kupakua programu hiyo na kuhifadhi machapisho mbalimbali katika kifaa chake

  • Tumia sehemu ya kutafuta ili upate mstari wa Biblia unaohitaji

  • Onyesha video. Ikiwa mwenye nyumba ana watoto, waonyeshe moja ya video za Uwe Rafiki ya Yehova. Au mwonyeshe mwenye nyumba video, Kwa Nini Ujifunze Biblia? ili kumchochea ajifunze Biblia. Ikiwa unayemhubiria anazungumza lugha nyingine, mwonyeshe video katika lugha yake

  • Mwonyeshe mtu andiko kutoka katika Biblia ya lugha nyingine uliyopakua mapema. Fungua andiko hilo, ubofye namba ya mstari, kisha bofya alama ya tafsiri za Biblia ili kusoma mstari huohuo katika lugha hiyo