1 Timotheo 2:1-15
2 Kwa hiyo ninahimiza, kwanza kabisa, kwamba dua, sala,+ maombezi, kutoa shukrani, yafanywe kwa ajili ya watu wa namna zote,+
2 kwa ajili ya wafalme+ na wale wote walio katika cheo cha juu;+ ili tuendelee kuishi maisha shwari na matulivu pamoja na ujitoaji-kimungu kamili na kuchukua mambo kwa uzito.+
3 Hili ni zuri nalo linakubalika+ machoni pa Mwokozi wetu, Mungu,+
4 ambaye mapenzi yake ni kwamba watu wa namna zote+ waokolewe+ na kupata ujuzi sahihi+ wa kweli.+
5 Kwa maana kuna Mungu mmoja,+ na mpatanishi+ mmoja kati ya Mungu+ na wanadamu,+ mwanadamu, Kristo Yesu,+
6 aliyejitoa kuwa fidia inayolingana kwa ajili ya wote+—hili ndilo litakalotolewa ushahidi kwenye nyakati zake maalumu.
7 Kwa kusudi la ushahidi+ huo mimi niliwekwa rasmi kuwa mhubiri na mtume+—ninasema kweli,+ sisemi uwongo—mwalimu wa mataifa+ katika jambo linalohusu imani+ na kweli.
8 Kwa hiyo natamani kwamba kila mahali wanaume waendelee kutoa sala, wakiinua mikono+ yenye ushikamanifu, bila ghadhabu+ na mabishano.+
9 Vivyo hivyo natamani wanawake wajipambe kwa mavazi yenye mpangilio mzuri, pamoja na kiasi+ na utimamu wa akili, si kwa mitindo ya kusuka nywele na dhahabu au lulu au mavazi yaliyo ghali sana,+
10 bali kwa njia inayowafaa wanawake wanaodai kumheshimu Mungu,+ yaani, kupitia matendo mema.+
11 Mwanamke na ajifunze akiwa kimya na kwa kujitiisha kikamili.+
12 Simruhusu mwanamke kufundisha,+ wala kuwa na mamlaka juu ya mwanamume,+ bali kuwa kimya.
13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Hawa.+
14 Pia, Adamu hakudanganywa,+ bali yule mwanamke alidanganywa+ kabisa naye akaingia katika kosa.+
15 Hata hivyo, mwanamke atabaki salama kupitia kuzaa watoto,+ bora tu waendelee katika imani na upendo na utakaso pamoja na utimamu wa akili.+