1 Timotheo 5:1-25
5 Usimkemee kwa ukali mwanamume mzee.+ Badala yake, msihi kama baba, wanaume vijana kama ndugu,
2 wanawake wazee+ kama mama, wanawake vijana kama dada+ kwa usafi wote wa kiadili.
3 Waheshimu wajane ambao ni wajane kwelikweli.+
4 Lakini ikiwa mjane yeyote ana watoto au wajukuu, acha hao wajifunze kwanza kuzoea ujitoaji-kimungu nyumbani+ kwao wenyewe na kuendelea kuwalipa wazazi+ na wazazi wa wazazi wao malipo yanayowastahili, kwa maana hilo linakubalika machoni pa Mungu.+
5 Basi mwanamke ambaye kwa kweli ni mjane na aliyeachwa maskini+ sana ameweka tumaini lake kwa Mungu+ naye anadumu katika dua na sala usiku na mchana.+
6 Lakini mwanamke anayejiingiza katika tamaa za mwili+ amekufa+ ingawa yuko hai.
7 Kwa hiyo endelea kutoa amri hizi,+ ili wasiwe wenye kulaumika.+
8 Hakika ikiwa yeyote hawaandalii mahitaji wale walio wake mwenyewe,+ na hasa wale walio washiriki wa nyumba yake,+ ameikana+ imani+ naye ni mbaya kuliko mtu asiye na imani.
9 Na mjane ambaye amekuwa mwenye umri usiopungua miaka 60, mke wa mume mmoja, awekwe katika orodha,+
10 mwenye kutolewa ushahidi juu ya matendo yaliyo mazuri,+ ikiwa alilea watoto,+ ikiwa alipokea wageni,+ ikiwa aliosha miguu ya watakatifu,+ ikiwa aliwasaidia wale walio katika dhiki,+ ikiwa alifuata kwa bidii kila tendo jema.+
11 Kwa upande mwingine, wakatae wanawake wajane ambao ni vijana, kwa maana tamaa zao za ngono zinapokuja kati yao na Kristo,+ wao hutaka kuolewa,
12 wakiwa na hukumu kwa sababu wamepuuza wonyesho wao wa kwanza wa imani.+
13 Wakati huohuo wao hujifunza pia kutokuwa na kazi, wakizunguka-zunguka nyumba kwa nyumba; ndiyo, si kwamba hawana kazi tu, bali pia ni wenye kupiga porojo na wenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine,+ wakiongea juu ya mambo ambayo hawapaswi.
14 Kwa hiyo natamani wanawake wajane ambao ni vijana waolewe,+ wazae watoto,+ wasimamie nyumba, wasimpe yule mpinzani sababu yoyote ya kutukana.+
15 Kwa kweli, tayari wengine wamegeuzwa kando kumfuata Shetani.
16 Ikiwa mwanamke yeyote mwamini ana wajane, acha yeye awasaidie wao,+ na acha kutaniko lisiwe chini ya mzigo huo. Ndipo liweze kuwasaidia wale ambao ni wajane kwelikweli.+
17 Wanaume wazee wanaosimamia+ kwa njia nzuri wahesabiwe kustahili heshima+ mara mbili, hasa wale wanaofanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.+
18 Kwa maana andiko linasema: “Hupaswi kumfunga kinywa ng’ombe-dume anapopura nafaka”;+ pia: “Mfanyakazi anastahili mshahara wake.”+
19 Usikubali shtaka juu ya mwanamume mzee, isipokuwa tu kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.+
20 Watu walio na mazoea ya kutenda dhambi+ uwakaripie+ mbele ya watazamaji, ili wengine pia waogope.+
21 Nakuagiza kwa uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu+ na malaika waliochaguliwa kwamba uyashike mambo haya bila kuhukumu mapema, bila kufanya jambo lolote kwa mwelekeo wenye ubaguzi.+
22 Usiweke kamwe mikono+ yako juu ya mtu yeyote haraka-haraka; wala usiwe mshiriki katika dhambi za wengine;+ jihifadhi ukiwa safi kiadili.+
23 Usiendelee kunywa maji, bali utumie divai+ kidogo kwa ajili ya tumbo lako na ugonjwa wako wa mara kwa mara.
24 Dhambi za watu wengine huwa wazi+ mbele ya watu wote, zikiongoza moja kwa moja kwenye hukumu, lakini kwa habari ya watu wengine pia dhambi zao huwa wazi baadaye.+
25 Vivyo hivyo pia matendo mazuri huwa wazi+ mbele ya watu wote na yale ambayo ni kinyume hayawezi kuendelea kufichwa.+