Hamia kwenye habari

Ndugu Rasul Rozbayev

MACHI 23, 2021
TURKMENISTAN

Ndugu Rasul Rozbayev Mwenye Umri wa Miaka 21 Afungwa kwa Mara ya Pili kwa Kukataa Kujiunga na Jeshi

Ndugu Rasul Rozbayev Mwenye Umri wa Miaka 21 Afungwa kwa Mara ya Pili kwa Kukataa Kujiunga na Jeshi

Hukumu Inatarajiwa

Machi 16, 2021, Mahakama ya Turkmenistan ilitangaza hukumu katika kesi kumhusu Ndugu Rasul Rozbayev. Amehukumiwa miaka miwili gerezani kwa kukataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya dhamiri. Hii ndiyo mara ya pili anafungwa kwa sababu ya msimamo wake wa kutounga mkono upande wowote.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Rasul Rozbayev

  • Alizaliwa: 1999 (Khallang)

  • Maisha Yake: Ana dada wawili wenye umri mkubwa kuliko yenye na mdogo wake mmoja wa kiume. Baada ya kumaliza shule ya sekondari alianza kujifunza jinsi ya kuwa kinyozi. Anapenda kucheza mpira wa miguu na wa wavu, na pia anapenda kuogelea

    Wazazi wake walibatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova alipokuwa mtoto. Alibatizwa mwaka wa 2013

Historia ya kesi

Desemba 19, 2017, Ndugu Rasul Rozbayev alihukumiwa kwa mara ya kwanza kwa kukataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya dhamiri. Alipewa miaka miwili ya utumishi wa kurekebisha tabia. Aligawiwa kipande cha ardhi ili alime ngano, na alipaswa kupeleka asilimia 20 ya mazao serikalini. Eneo alilopewa liko mbali sana na nyumbani. Kwa sababu hana gari, alilazimika kutembea hadi huko.

Kulingana na sheria ya Turkmenistan, wenye mamlaka wanaweza kumhukumu mtu kwa mara ya pili ikiwa anakataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya dhamiri. Hivyo, Aprili 22, 2020, aliripoti tena kwenye ofisi ya kuwaandikisha wanajeshi na kukataa kujiunga na jeshi. Kwa sababu hiyo alipaswa kuripoti mara kadhaa kwenye ofisi ya jeshi, kuhojiawa, kupimwa afya, na kutishwa kwamba atashtakiwa, na mambo hayo yaliendelea kwa miezi kadhaa. Januari 22, 2021, kesi yake ilifikishwa mbele ya mwendesha-mashtaka.

Rasul amepata ujasiri kwa kujifunza kutokana na mifano ya ndugu na dada wengine wanaokabili changamoto kama zake. Anasema hivi: “Mifano yao inanisaidia kumtegemea Yehova . . . na inanitia nguvu ninapokabili majaribu. Nitawafurahisha Yehova na Yesu ikiwa nitaendelea kuwa mwaminifu.” Hali yake pia imejaribu imani ya familia yake yote. Mama yake anaeleza kinachomsaidia kuwa imara katika kipindi hiki: “Nilijifunza kutokana na mifano ya Biblia na kutoka kwenye video zetu kwamba si mimi tu ninayekabili jaribu la aina hii. Ndugu na dada wengine pia wameteswa, nao wamefaulu kuwa washindi. Mifano yao inaniimarisha ili niweze kuvumilia.”

Rasul amepata faraja kupitia maneno yaliyo kwenye Zaburi 37:23, 24. Kwa msaada wa Yehova, tunajua kwamba Rasul pamoja na vijana wengine jasiri watadumisha imani, ushikamanifu, na shangwe yao.