Hamia kwenye habari

Nyumba ya ndugu mmoja iliyoharibiwa na tetemeko la ardhi nchini Haiti

AGOSTI 18, 2021
HAITI

Tetemeko Kubwa la Ardhi Laipiga Haiti

Tetemeko Kubwa la Ardhi Laipiga Haiti

Agosti 14, 2021, tetemeko la ardhi lenye kipimo cha 7.2 lilikumba eneo la kusini-magharibi mwa Haiti, likifuatiwa na matetemeko mengine madogo. Bado uharibifu unaendelea kukaguliwa.

Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata

  • Kwa kusikitisha, dada 2 na ndugu 1 walikufa

  • Ndugu na dada 21 wamejeruhiwa

  • Nyumba 119 zimeharibiwa

  • Nyumba 72 zimeharibika kabisa

  • Majumba 5 ya Ufalme yamepata uharibifu mdogo

  • Majumba 4 ya Ufalme yameharibiwa sana

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Halmashauri ya Kutoa Msaada (DRC) inaongoza kazi ya kutoa msaada. DRC inafanya kazi na waangalizi 2 wa mzunguko katika eneo lililoathiriwa pamoja na wazee wa eneo hilo ili kuandaa msaada na uchungaji

  • DRC inasimamia kugawanywa kwa misaada ya kibinadamu, kama vile blanketi, mavazi, chakula, dawa, maturubai, na maji. Pia wamefanya mipango ili ndugu na dada waliojeruhiwa wapate msaada wa kitiba

  • Jitihada zote za kutoa msaada zinafanywa kupatana na miongozo ya kujilinda na COVID-19

Licha ya hali ngumu, makutaniko mengi katika eneo lililoathiriwa yalifaulu kuwa na mikutano ya mwisho juma kupitia video iliyounganishwa kwenye mtandao Jumapili, Agosti 15. Pia, ndugu na dada waliweza kutazama programu ya Jumapili asubuhi ya Kusanyiko la Eneo la “Uwe Mwenye Nguvu kwa Imani.”

Tunasikitika kwa kuwapoteza waabudu wenzetu katika kifo. Tunasali kwa ajili ya ndugu na dada ambao wanaomboleza au kuteseka kimwili na kihisia kutokana na tetemeko hili la ardhi. Tunajua kwamba Yehova anaona uchungu wao naye ataendelea kuwa kimbilio lao na kuwapa nguvu katika kipindi hiki cha taabu.—Zaburi 46:1, 2.