Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | KIFO NDIO MWISHO WA MAMBO YOTE?

Kifo Si Mwisho wa Mambo Yote!

Kifo Si Mwisho wa Mambo Yote!

Bethania kilikuwa kijiji kidogo kilichokuwa kwenye umbali wa kilometa 3 na Yerusalemu. (Yohana 11:18) Musiba ulitokea katika kijiji hicho majuma machache mbele ya kifo cha Yesu. Lazaro, mumoja kati ya marafiki wa nguvu wa Yesu, aligonjwa sana bila kutazamia na akakufa.

Wakati Yesu alisikia habari hiyo mara ya kwanza aliwaambia wanafunzi wake kwamba Lazaro analala na kwamba ataenda huko ili kumuamusha. (Yohana 11:11) Lakini wanafunzi wa Yesu hawakuelewa maana ya maneno hayo, kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi hivi: “Lazaro amekufa.”​—Yohana 11:14.

Siku ine kisha Lazaro kuzikwa, Yesu alifika Bethania na alipenda kumufariji Martha, dada ya Lazaro. Martha akasema hivi: “Kama ungekuwa hapa ndugu yangu hangekufa.” (Yohana 11:17, 21) Yesu akajibu hivi: “Mimi ndiye ufufuo na uzima. Yule anayeniamini, hata akifa, atarudi kwenye uzima.”​—Yohana 11:25.

‘Lazaro, kuja huku inje!’

Ili kuonyesha kwamba maneno hayo yalikuwa ya kweli, Yesu alikaribia kaburi na akaita kwa kusema hivi: ‘Lazaro, kuja huku inje!’ (Yohana 11:43) Na kwa mushangao wa watazamaji, yule mutu aliyekuwa amekufa akatoka katika kaburi.

Mbele ya ufufuo wa Lazaro, Yesu alikuwa amefufua watu wawili. Wakati mumoja, alifufua kijana mwanamuke, ni kusema, binti ya Yairo. Mbele tu ya kumufufua kijana huyo, Yesu alieleza pia kuwa kijana huyo alikuwa analala.​—Luka 8:52.

Jua kwamba kuhusu kifo cha Lazaro na kifo cha binti ya Yairo, Yesu alilinganisha kifo na usingizi. Huo ni ulinganifu wenye kufaa kabisa. Sababu gani? Usingizi ni hali ya kutojua kitu chochote na hali hiyo inaonyesha vizuri kwamba mutu aliyekufa hasikie maumivu na hateseke. (Mhubiri 9:5; soma kisanduku,  “Kifo Ni Kama Usingizi Muzito.”) Wanafunzi wa kwanza wa Yesu walielewa vizuri hali ya kweli ya wafu. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Wafuasi waliona kifo kuwa usingizi, na kaburi palikuwa mahali pa kupumuzika . . . kwa wale waliokufa katika imani.” * (Encyclopedia of Religion and Ethics)

Tunafarijiwa kujua kwamba wafu wanalala usingizi katika kaburi na hawateseke. Kwa hiyo, tunajua jambo linalotokea tunapokufa na hatuhitaji tena kuogopa kifo.

‘MUTU AKIFA, JE, ANAWEZA KUISHI TENA?’

Ijapokuwa tunafurahia kulala usingizi muzuri usiku, ni nani anaweza kupenda alale usingizi milele? Je, kuna tumaini kwamba watu wanaolala usingizi katika kaburi wataishi tena kama Lazaro na binti ya Yairo?

Ayubu, muzee wa ukoo, aliuliza hivi alipokaribia kufa: ‘Mutu akifa, je, anaweza kuishi tena?’​—Ayubu 14:14.

Akizungumuza na Mungu Mweza​-Yote, Ayubu alijibu ulizo lake mwenyewe kwa kusema hivi: “Wewe utaita, na mimi mwenyewe nitakujibu. Kwa kuwa utaitamani sana kazi ya mikono yako.” (Ayubu 14:15) Ayubu alikuwa hakika kwamba Yehova alitamani kuona siku ambayo atafufua mutumishi wake muaminifu. Je, Ayubu alitamani jambo fulani ambalo haliwezi kufanyika? Hapana.

Ufufuo mbalimbali ambao Yesu alifanya ulihakikisha wazi kwamba Mungu alimupatia Yesu uwezo wa kushinda kifo. Kwa kweli, Biblia inasema kwamba sasa Yesu ana “funguo za kifo.” (Ufunuo 1:18) Kama vile Yesu alivyokuwa na uwezo wa kumufufua Lazaro, ana uwezo wa kuwafufua watu wakati unaokuja.

Biblia inazungumuzia mara nyingi ahadi hiyo. Malaika alimuhakikishia nabii Danieli hivi: ‘Utapumuzika, lakini utasimama kwa ajili ya fungu lako mwishoni mwa zile siku.’ (Danieli 12:13) Yesu aliwaambia hivi Masadukayo, viongozi Wayahudi waliokataa ahadi ya ufufuo: ‘Ninyi munakosea, kwa sababu hamujue Maandiko wala nguvu za Mungu.’ (Mathayo 22:23, 29) Mutume Paulo alisema hivi: “Nina tumaini kwa Mungu . . . ya kwamba utakuwa ufufuo wa wafu, wenye haki na wasio haki pia.”​—Matendo 24:15, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo.

WATU WALIOKUFA WATAFUFULIWA WAKATI GANI?

Ufufuo huo wa wenye haki na wasio haki utakuwa wakati gani? Malaika alimuambia Danieli, mutu mwenye haki, kwamba atafufuliwa “mwishoni mwa zile siku.” Martha aliamini pia kwamba ndugu yake Lazaro, ‘angefufuka katika ufufuo siku ya mwisho.’​—Yohana 11:24.

Biblia inasema kuwa “siku za mwisho” zilianza wakati Kristo alianza kutawala akiwa Mufalme. Paulo aliandika hivi: ‘Kwa maana ni lazima Kristo atawale akiwa mufalme mupaka Mungu awe ameweka adui zote chini ya miguu yake. Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.’ (1 Wakorintho 15:25, 26) Hiyo ndiyo sababu kubwa tunapaswa kuomba Ufalme wa Mungu uje na mapenzi ya Mungu yafanyike hapa duniani. *

Kama tu Ayubu alivyojua, mapenzi ya Mungu ni kuwafufua watu waliokufa. Wakati siku hiyo itafika, kifo kitamalizwa kabisa. Na hakuna mutu atakayejiuliza tena, ‘Kifo ndio mwisho wa mambo yote?’

^ Neno la Kiswahili “kaburi” linatokana na neno la Kigiriki linalomaanisha “mahali pa kupumuzika.”

^ Ili kupata habari zingine juu ya Ufalme wa Mungu, usome sura ya 8 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Unaweza pia kupata kitabu hicho kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org.