Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | KIFO NDIO MWISHO WA MAMBO YOTE?

Wanadamu Wanapiganisha Kifo

Wanadamu Wanapiganisha Kifo

MUFALME QIN SHI HUANG

MUVUMBUZI PONCE DE LEÓN

Kifo ni adui mwenye kuogopesha sana. Tunamupiganisha adui huyo kwa nguvu zetu zote. Mutu fulani tunayependa anapokufa, wakati mwengine ni vigumu kukubali kwamba jambo hilo limetokea. Ao, wakati tungali na nguvu za ujana tunaweza kufikiri kwamba hatutakufa hata siku moja, wazo la uongo ambalo tunajikaza kushikilia sana.

Mafarao wa zamani wa Misri ndio waliofikiri zaidi juu ya kuishi bila kufa kuliko watu wengine wote. Walitumia sehemu kubwa ya maisha yao wenyewe, na hata maisha ya maelfu ya watumishi wao ili kujaribu kushinda kifo. Mapiramidi waliyojenga yanahakikisha kile walikuwa wanatafuta na namna walivyoshindwa kukipata.

Wafalme wa China walitafuta pia kupiganisha kifo, lakini walitumia njia nyingine, ni kusema, walitengeneza madawa ambayo yaliwaziwa kuwa yanarefusha uzima. Mufalme Quin Shi Huang aliwaomba mafundi wake wamutengenezee dawa ya kuzuia kifo. Lakini madawa mengi kati ya madawa waliyotengeneza yalikuwa na zebaki (mercure) yenye sumu, na labda moja kati ya madawa hayo yaliyochanganywa ndiyo ilimuua.

Katika mwaka wa 1513 kisha kuzaliwa kwa Yesu, muvumbuzi Muhispania Juan Ponce de León alisafiri mara nyingi kwa meli mupaka Karibea ili kutafuta chemchemi ya ujana. Alivumbua eneo la Florida katika Amerika, lakini alikufa katika safari hiyo kisha mapigano pamoja na watu wa Amerika. Na hakuna chemchemi yoyote ya ujana ambayo imekwisha kupatikana.

Mafarao wa Misri, wafalme wa China, na wavumbuzi, wote walitafuta kushinda kifo. Ni nani kati yetu anayeweza kuzarau muradi wao, hata ikiwa hatupendezwe na njia walizotumia? Ndani ya moyo wetu, sisi wote tunatamani kuendelea kuishi.

KIFO KINAWEZA KUSHINDWA?

Sababu gani tunapiganisha kifo? Biblia inaeleza sababu. Kuhusu Muumbaji wetu, Yehova Mungu, * Biblia inasema hivi: “Amefanya kila kitu kiwe chenye kupendeza kwa wakati wake. Tena wakati usio na kipimo ameuweka ndani ya moyo [wa wanadamu].” (Mhubiri 3:11) Tungependa kufurahia uzuri wa dunia milele, si tu kwa miaka 80 hivi ao zaidi. (Zaburi 90:10) Hiyo ndiyo tamaa ya moyo wetu.

Sababu gani Mungu aliweka “wakati usio na kipimo” ndani ya moyo wetu? Je, alifanya hivyo ili tu kutuvunja moyo? Hatuwezi kuwaza hivyo. Tofauti na hilo, Mungu anatuahidi kwamba kifo kitashindwa. Biblia inazungumuza mara nyingi juu ya kuondolewa kwa kifo na ahadi ya Mungu ya uzima wa milele.​—Soma kisanduku,  “Kifo Kitashindwa.”

Yesu Kristo mwenyewe alisema waziwazi hivi: ‘Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemutuma, Yesu Kristo.’ (Yohana 17:3) Kwa hiyo, kupiganisha kifo si pigano lisilo na tumaini. Hata hivyo, Yesu alihakikisha kuwa ni Mungu tu ndiye anaweza kutushindia pigano hilo.

^ Yehova ni jina la Mungu kama inavyoonyeshwa katika Biblia.