Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Ni katika maana gani kifo cha washikamanifu ni ‘chenye samani machoni pa Yehova’?

▪ Akiongozwa na roho ya Mungu, mutunga​-zaburi aliimba hivi: ‘Ni chenye samani machoni pa Yehova, kifo cha washikamanifu wake.’ (Zab. 116:15) Uzima wa kila mwabudu wa kweli wa Yehova ni wa bei sana kwake. Hata hivyo, maneno ya Zaburi 116 hayazungumuzie tu kifo cha mutumishi mumoja wa Yehova.

Wakati wa hotuba ya maziko, haifai kutumia Zaburi 116:15 juu ya mutu aliyekufa, hata ikiwa alikufa akiwa mwaminifu kwa Yehova. Sababu gani? Kwa sababu maneno hayo ya mutunga​-zaburi hayazungumuzie tu kifo cha mutu mumoja. Maneno hayo yanamaanisha kama kifo cha watumishi wote wa Yehova waaminifu ni chenye bei sana machoni pake hivi kwamba hawezi kuruhusu watumishi wake wote wakufe.​—Ona Zaburi 72:14; 116:8.

Andiko la Zaburi 116:15 linatuhakikishia kama Yehova hataruhusu watumishi wake wote kwa ujumla waangamizwe ili wasiwe tena duniani. Kwa kweli, historia yetu ya sasa inaonyesha ukweli huo. Mashahidi wa Yehova wamevumilia taabu na mateso makali, hilo linaonyesha waziwazi kama Mungu hawezi kuruhusu sisi wote tuangamizwe.

Kwa kuwa Yehova ana nguvu zote na anatimiza siku zote ahadi zake, yeye hataruhusu tuangamizwe sisi wote kwa ujumla. Ikiwa Mungu angeruhusu jambo hilo litokee, hilo lingeonyesha kama maadui wake wana nguvu kuliko yeye, jambo ambalo haliwezakani! Kusudi la Yehova ni kwamba dunia ikaliwe na watu walio waaminifu kwake. Sasa ikiwa watumishi wake wote wanaangamizwa, kusudi hilo litamizwa namna gani? Kwa hiyo, hilo ni jambo lisilowezekana. (Isa. 45:18; 55:10, 11) Haiwezekani kabisa, kwa sababu watumishi wake wote wakiangamizwa, hakutakuwa na mutu duniani atakayemutolea utumishi mutakatifu na kumuabudu katika viwanja vya hekalu lake kubwa la kiroho. Tena, hakutakuwa watu ambao wataunda ‘dunia mupya,’ yaani, watu wenye haki watakaotawaliwa na ‘mbingu mupya.’ (Ufu. 21:1) Jambo hilo likitendeka, Yesu atakosa watu wa kutawala wakati wa Utawala wake wa Miaka Elfu.​—Ufu. 20:4, 5.

Mungu akiruhusu maadui wake waondoe kabisa watumishi wake wote duniani, atachekelewa na kuonwa kuwa yeye si Mungu. Tena, hilo lingeonyesha kama Yehova hastahili kuitwa Mutawala Mukubwa wa Ulimwengu Wote Muzima. Zaidi ya hilo, kwa sababu ya heshima anayostahili na kwa sababu ya jina lake takatifu, Yehova hataruhusu watumishi wake wote kwa ujumla waangamizwe duniani. Fikiria hili: Kwa kuwa Mungu “hana ukosefu wowote wa haki,” yeye hawezi hata kidogo kushindwa kuwalinda watu ambao wamekuwa wakimutumikia kwa uaminifu. (Kum. 32:4; Mwa. 18:25) Pia, akiruhusu watumishi wake wote waangamizwe, hilo halitapatana na Neno la Mungu linalosema: “Yehova hatawaacha watu wake kwa ajili ya jina lake kuu.” (1 Sam. 12:22) Hakika, ‘Yehova hatawaacha watu wake, wala hatauacha uriti wake mwenyewe.’​—Zab. 94:14.

Inatuliza moyo sana kujua kama watu wa Yehova hawawezi hata kidogo kuangamizwa wote ili wasionekane tena duniani. Kwa hiyo basi, siku zote tuendelee kuwa waaminifu kwa Mungu na kutumaini ahadi yake inayosema: ‘Silaha yoyote itakayofanywa juu yako haitafanikiwa, na ulimi wowote utakaoinuka juu yako katika hukumu wewe utauhukumu. Hilo ndilo fungu la uriti la watumishi wa Yehova, na uadilifu wao ni kutoka kwangu.’​—Isa. 54:17.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 22]

Mungu hataruhusu hata kidogo watu wake wote waangamizwe