Kumbukumbu la Torati 32:1-52

  • Wimbo wa Musa (1-47)

    • Yehova ni Mwamba (4)

    • Israeli anamusahau Mwamba wake (18)

    • “Kisasi ni changu” (35)

    • “Mufurahi, ninyi mataifa, pamoja na watu wake” (43)

  • Musa atakufa juu ya Mulima Nebo (48-52)

32  “Mutege sikio, Enyi mbingu, na mimi nitasema,Na dunia isikie maneno ya kinywa changu.  2  Mafundisho yangu yataanguka kama mvua;Maneno yangu yataanguka matone-matone kama umande,Kama mvua ya kidogo-kidogo juu ya majaniNa kama matone mengi ya mvua juu ya mimea.  3  Kwa maana nitatangaza jina la Yehova.+ Museme kuhusu ukubwa wa Mungu wetu!+  4  Mwamba, kazi zake ni kamilifu,+Kwa maana njia zake zote ni haki.+ Mungu wa uaminifu+ mwenye hana ukosefu wa haki hata kidogo;+Yeye ni mwenye haki na munyoofu.+  5  Wao ndio wametenda kwa upotovu.+ Hawako watoto wake, kasoro ni yao wenyewe.+ Wao ni kizazi chenye kuharibika na chenye kupotoka!+  6  Je, ni hivi munapaswa kumutendea Yehova,+Enyi wapumbavu na wenye kukosa hekima?+ Je, yeye haiko Baba yenu mwenye aliwaumba,+Je, haiko Yeye ndiye aliwafanya na kuwaimarisha kabisa?  7  Kumbuka siku za zamani;Mufikirie miaka ya vizazi vyenye vimepita. Uliza baba yako, na atakuambia;+Wazee wako, na watakujulisha.  8  Wakati Mwenye Kuwa Juu Zaidi alipatia mataifa uriti wao,+Wakati alitenganisha wana wa Adamu,*+Aliweka mupaka wa vikundi vya watu+Kulingana na hesabu ya wana wa Israeli.+  9  Kwa maana watu wa Yehova ni fungu lake;+Yakobo ni uriti wake.+ 10  Alimupata katika inchi yenye jangwa+Na katika jangwa tupu, lenye milio.+ Alimuzunguka ili kumulinda, akamutunza,+Na kumulinda kama mboni ya jicho lake.+ 11  Kama vile tai anatikisa chicha yake,*Anapanda juu ya vitoto vyake,Akinyoosha mabawa yake, na kuvikamata,Akivibeba juu ya mabawa yake,+ 12  Yehova peke yake aliendelea kumuongoza;*+Hakuna mungu yeyote wa kigeni mwenye alikuwa pamoja naye.+ 13  Alimupitisha juu ya sehemu za juu za dunia,+Na hivyo akakula mazao ya mashamba.+ Alimukulisha asali kutoka katika mwambaNa mafuta kutoka katika jiwe ngumu, 14  Siagi ya mifugo na maziwa ya kundi,Pamoja na kondoo wazuri sana,*Na kondoo-dume wa Bashani, na mbuzi-dume,Pamoja na ngano ya muzuri sana;*+Na ulikunywa divai kutoka katika damu* ya zabibu. 15  Wakati Yeshuruni* alinenepa, alipiga-piga muguu kwa uasi. Umenenepa, umekuwa na mafuta mengi katika mwili, tumbo lako limenenepa.+ Kwa hiyo akamuacha Mungu, mwenye alimufanya,+Na akamuzarau Mwamba wa wokovu wake. 16  Waliamusha kasirani yake kali kupitia miungu ya kigeni;+Walikuwa wanamukasirisha na mambo yenye kuchukiza.+ 17  Walikuwa wanatoa zabihu kwa pepo wachafu, hapana kwa Mungu,+Kwa miungu yenye hawakujua,Mipya yenye ilikuja sasa hivi,Kwa miungu yenye mababu zenu hawakujua. 18  Ulimusahau Mwamba,+ baba yako mwenye alikuzaa,Na haukumukumbuka Mungu mwenye alikuzaa.+ 19  Wakati Yehova aliona jambo hilo, aliwakataa+Kwa sababu watoto wake wanaume na watoto wake wanamuke walimukasirisha. 20  Kwa hiyo akasema, ‘Nitaficha uso wangu wasiuone;+Nitaona chenye kitawapata. Kwa maana wao ni kizazi chenye kupotoka,+Wana wenye hakuna uaminifu ndani yao.+ 21  Wameamusha kasirani yangu kali* kwa kitu chenye hakiko mungu;+Wamenikasirisha kwa sanamu zao zenye hazina mafaa yoyote.+ Kwa hiyo nitawachochea wakuwe na wivu kupitia wale wenye hawako kikundi cha watu;+Nitawakasirisha kwa kutumia taifa pumbavu.+ 22  Kwa maana kasirani yangu imewaka moto+Wenye utateketeza mupaka kwenye sehemu za chini kabisa za Kaburi,*+Na utateketeza dunia na mazao yakeNa kuchoma misingi ya milima. 23  Nitaongeza misiba yao;Nitawapiga kwa mishale yangu mupaka iishe. 24  Watachoka kwa sababu ya njaa+Na kukuliwa na homa kali na uharibifu muchungu.+ Nitawatumia meno ya wanyama ili yawashambulie+Na sumu ya wanyama wenye kutambaa katika mavumbi. 25  Inje, upanga utawaacha mikono wazi;+Ndani, kuko woga mukubwa+Kwa kijana mwanaume na bikira,Mutoto mwenye kunyonya pamoja na muzee mwenye imvi.+ 26  Ningesema: “Nitawasambaza;Nitafanya kumbukumbu lao lisahauliwe kati ya wanadamu,” 27  Haingekuwa kwa sababu ya kuogopa namna adui yangu atatenda,+Kwa sababu wapinzani wanaweza kulielewa mubaya,+Wanaweza kusema: “Nguvu zetu zimeshinda;+Haiko Yehova ndiye alifanya mambo haya yote.” 28  Kwa maana wao ni taifa lenye kukosa akili,*Na hakuna uelewaji kati yao.+ 29  Kama tu wangekuwa na hekima!+ Wangefikiri sana juu ya jambo hili.+ Wangewaza kuhusu mwisho wao.+ 30  Namna gani mutu mumoja angeweza kufuatilia elfu moja (1 000),Na wawili kukimbiza elfu kumi (10 000)?+ Haingewezekana kama Mwamba wao hangekuwa amewauzisha+Na kama Yehova hangewatia katika mukono wa maadui. 31  Kwa maana mwamba wao haiko kama Mwamba wetu,+Hata maadui wetu wameelewa jambo hilo.+ 32  Kwa maana muzabibu wao unatoka katika muzabibu wa SodomaNa kutoka katika matuta ya Gomora.+ Zabibu zao ni zabibu za sumu,Vishada vyao ni vichungu.+ 33  Divai yao ni sumu ya nyoka,Sumu kali ya nyoka-kobra. 34  Je, hili haliwekwe karibu na mimi,Halifungwe kwa muhuri katika depo yangu?+ 35  Kisasi ni changu, na malipo,+Kwa wakati wenye kuwekwa wakati muguu wao utatereza,+Kwa maana siku ya musiba wao iko karibu,Na chenye kinawangojea kitafika haraka.’ 36  Kwa maana Yehova atahukumu watu wake,+Na atasikilia huruma* watumishi wake+Wakati ataona kwamba nguvu zao zimeisha,Na kwamba wenye hawana uwezo na wenye kuwa wazaifu tu ndio wamebakia. 37  Halafu atasema, ‘Miungu yao iko wapi,+Mwamba wenye walikimbilia, 38  Yenye ilikuwa inakula mafuta ya zabihu zao,*Kunywa divai ya matoleo yao ya kinywaji?+ Isimame na kuwasaidia ninyi. Ikuwe mahali penu pa kukimbilia. 39  Sasa muangalie kwamba mimi⁠—​mimi ndiye,+Na hakuna miungu mingine isipokuwa mimi.+ Mimi ninaua, na mimi ninafanya kuwa muzima.+ Ninaumiza,+ na nitaponyesha,+Na hakuna mwenye anaweza kuokoa katika mukono wangu.+ 40  Kwa maana ninainua mukono wangu mbinguni,Na ninaapa: “Kama vile hakika ninaishi milele,”+ 41  Kama ninanoa upanga wangu wenye kumetametaNa kutayarisha mukono wangu kwa ajili ya hukumu,+Nitalipiza kisasi juu ya maadui wangu+Na kuwalipa wale wenye kunichukia. 42  Nitalewesha mishale yangu kwa damu,Na upanga wangu utakula nyama,Pamoja na damu ya wenye waliuawa na pia watu wenye walikamatwa mateka,Pamoja na vichwa vya viongozi wa adui.’ 43  Mufurahi, ninyi mataifa, pamoja na watu wake,+Kwa maana atalipizia kisasi damu ya watumishi wake,+Na atalipiza kisasi maadui wake+Na atafunika zambi kwa ajili ya* inchi ya watu wake.” 44  Basi Musa akakuja na kurudilia-rudilia maneno yote ya wimbo huo katika masikio ya watu,+ yeye na Hoshea*+ mwana wa Nuni. 45  Kisha Musa kumaliza kuambia Israeli wote maneno hayo yote, 46  akawaambia: “Muweke katika moyo wenu maonyo yote yenye ninawapatia leo,+ ili muamuru wana wenu wakuwe waangalifu kufanya maneno yote ya Sheria hii.+ 47  Kwa maana hili haliko neno lenye halina maana kwenu, lakini linamaanisha uzima wenu,+ na kupitia neno hili munaweza kuishi wakati murefu katika inchi yenye munavuka Yordani ili kuiriti.” 48  Yehova akasema na Musa siku ileile, na kumuambia: 49  “Panda juu ya mulima huu wa Abarimu,+ Mulima Nebo,+ wenye kuwa katika inchi ya Moabu, wenye unaangaliana na Yeriko, na uangalie inchi ya Kanaani, yenye ninapatia Waisraeli kuwa mali yao.+ 50  Kisha utakufa juu ya mulima wenye utapanda sasa hivi, na utakusanywa kwa watu wako,* kama vile Haruni ndugu yako alikufa juu ya Mulima Hori+ na akakusanywa kwa watu wake, 51  kwa sababu ninyi wote wawili hamukukuwa waaminifu kwangu kati ya Waisraeli kwenye maji ya Meriba+ ya Kadeshi katika jangwa la Zini, kwa sababu hamukunitakasa mbele ya watu wa Israeli.+ 52  Utaona inchi hiyo kwa mbali, lakini hautaingia katika inchi hiyo yenye ninapatia watu wa Israeli.”+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “jamii ya wanadamu.”
Ao “nyumba yake; kiota chake.”
Ni kusema, Yakobo.
Tnn., “mafuta ya kondoo.”
Tnn., “mafuta ya figo ya ngano.”
Ao “maji.”
Maana yake “Mutu Munyoofu,” jina la heshima la Israeli.
Ao “wivu wangu.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao pengine, “lenye halisikie shauri.”
Ao “atasikitika kwa sababu ya.”
Ao “inakula zabihu zao za muzuri sana.”
Ao “atasafisha.”
Jina la kwanza la Yoshua. Hoshea ni ufupisho wa jina Hoshaya, lenye kumaanisha “Mwenye Aliokolewa na Yah; Yah Ameokoa.”
Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.