Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Dini

Dini

Sababu gani kuna dini nyingi?

‘Munaiacha amri ya Mungu, na kuyashika sana mapokeo ya wanadamu.’—Marko 7:8.

MAWAZO YA BIBLIA

Watu wanazaliwa wakiwa na “uhitaji wa kiroho” ambao wanaweza kutosheleza kwa kumuabudu Mungu. (Mathayo 5:3) Ili wafikie kutosheleza uhitaji huo, watu wameunda dini nyingi ambazo zinategemea mawazo ya watu kuliko kutegemea mawazo ya Mungu.

Kwa mufano, Biblia inazungumuzia washiriki wa kikundi fulani cha dini katika siku za mitume: “Kwa maana nawatolea ushahidi kwamba wana bidii kwa ajili ya Mungu; lakini si kulingana na ujuzi sahihi. Kwa maana, kwa sababu ya kukosa kujua uadilifu wa Mungu bali wakitafuta kujiwekea uadilifu [ao haki] wao wenyewe, hawakujitiisha kwa uadilifu wa Mungu.” (Waroma 10:2, 3) Vilevile leo, kuna dini nyingi ambazo ‘zinafundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.’—Marko 7:7.

Je, ni lazima kuwa katika dini fulani?

‘Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe.’—Waebrania 10:24, 25.

MAWAZO YA BIBLIA

Andiko la Waebrania 10:25 linatumia maneno “bila kuacha kukusanyika pamoja.” Maneno hayo yanaonyesha kama Mungu anataka watu wakutane wakiwa kikundi ili kumuabudu. Lakini, je, kila muabudu anaweza kumujua Mungu na kujua mapenzi yake kwa namna yake? Hapana. Biblia inasema kwamba wale wanaomuabudu Mungu kwa njia ambayo anakubali wanapaswa ‘kusema kwa upatano na kuunganishwa vema katika akili ileile na katika njia ileile ya kufikiri.’ (1 Wakorintho 1:10) Ni lazima wapangwe katika makutaniko na ‘waupende ushirika muzima wa akina ndugu’ ulimwenguni pote. (1 Petro 2:17; 1 Wakorintho 11:16) Umoja katika ibada kama huo ni wa maana ili kumufurahisha Mungu.

Inawezekana kuitambua dini ya kweli?

‘Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mukiwa na upendo kati yenu wenyewe.’—Yohana 13:35.

MAWAZO YA BIBLIA

Ili kuonyesha namna tunaweza kuitambua dini ya kweli, Biblia inasema: ‘Kwa matunda yao mutawatambua. Je, watu wanakusanya zabibu kutoka kwenye miiba au tini kutoka kwenye michongoma?’ (Mathayo 7:16) Si lazima kuwa na ujuzi mwingi juu ya mimea ili kujua kutofautisha mutini na muti wenye miiba. Vilevile, si lazima kujua mengi juu ya mambo ya dini ili ujue kutofautisha dini ya kweli na ya uongo. Ni matunda ao mambo gani ambayo yanaweza kutusaidia tutambue ndini ya kweli?

  • Dini ya kweli inafundisha kweli inayotoka katika neno la Mungu, Biblia. (Yohana 4:24; 17:17) Mafundisho ya dini ya kweli hayategemee mawazo ya watu.

  • Dini ya kweli inasaidia watu kumujua Mungu na jina lake, Yehova.—Yohana 17:3, 6.

  • Dini ya kweli inafundisha kwamba Ufalme wa Mungu ndio utamaliza matatizo ya watu, si serikali za wanadamu.—Mathayo 10:7; 24:14.

  • Dini ya kweli inatia watu moyo wapendane. (Yohana 13:35) Inafundisha watu kuheshimia watu wa kabila na luga zote, kutumia wakati wao na mali zao ili kuwasaidia wengine, na kuepuka kujiingiza katika vita.—Mika 4:1-4.

  • Dini ya kweli ni njia ya maisha, si kufuata mambo kidesturi tu. Washiriki wa dini ya kweli wanatumikisha mambo ambayo wanafundisha.—Waroma 2:21; 1 Yohana 3:18.

Mashahidi wa Yehova, wachapishaji wa gazeti hili, wanajikaza kumutukuza Yehova kwa maneno na kwa matendo. Unaweza kufika kwenye mikutano yao kwenye Jumba la Ufalme ili ujionee jambo hilo!