SEHEMU YA 1
“Nguvu . . . Zenye Kuogopesha”
Katika sehemu hii tutachunguza masimulizi ya Biblia yanayothibitisha kwamba Yehova ana nguvu za kuumba, kuangamiza, kulinda, na kurudisha hali upya. Mioyo yetu itakuwa na ujasiri na tumaini tukielewa jinsi Yehova Mungu, mwenye ‘nguvu zenye kuogopesha’ anavyotumia “nguvu zake nyingi zenye msukumo.”—Isaya 40:26.
KATIKA SEHEMU HII
SURA YA 4
“Yehova . . . Ana Nguvu Nyingi”
Je, tunapaswa kumwogopa Mungu kwa sababu ya nguvu zake? Tunaweza kujibu swali hilo ndiyo na hapana.
SURA YA 5
Nguvu za Kuumba—“Muumba wa Mbingu na Dunia”
Kuanzia jua lililo kubwa sana mpaka ndege mvumaji, uumbaji wa Mungu unaweza kutufundisha jambo muhimu kumhusu.
SURA YA 6
Nguvu za Kuangamiza—“Yehova Ni Shujaa Mwenye Nguvu”
Ni kwa njia gani “Mungu wa amani” hupigana vita?
SURA YA 7
Nguvu za Kulinda—“Mungu ni Kimbilio Letu”
Mungu anawalinda watumishi wake kupitia njia mbili, lakini njia moja ni muhimu zaidi.
SURA YA 8
Uwezo wa Kurudisha Hali Nzuri—Yehova ‘Anafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya’
Tayari Yehova ameirudisha ibada safi. Atarudisha nini wakati ujao?
SURA YA 9
“Kristo Ni Nguvu za Mungu”
Miujiza na mafundisho ya Yesu Kristo yanaonyesha nini kumhusu Yehova?
SURA YA 10
“Iweni Waigaji wa Mungu” Mnapotumia Mamlaka
Una uwezo mkubwa kuliko unavyofikiri. Unawezaje kuutumia kwa njia inayofaa?

