SEHEMU YA KWANZA
“Mbingu Zilifunguliwa”
WAZO KUU: Maono ya makao ya Yehova
Hakuna mwanadamu anayeweza kumwona Mungu mweza yote, Yehova, naye aendelee kuishi. (Kut. 33:20) Hata hivyo, Yehova alimpa Ezekieli maono ambayo yanafunua sehemu ya kimbingu ya tengenezo Lake—maono ambayo yanatushangaza na pia yanatufanya tuthamini pendeleo la kumwabudu Mungu wa pekee wa kweli.
KATIKA SEHEMU HII
SURA YA 3
“Nikaanza Kuona Maono ya Mungu”
Maono ya kwanza ya Ezekieli yalimfanya alemewe kabisa. Mambo aliyoona yana maana kubwa kwa watumishi wa Mungu leo.
SURA YA 4
“Viumbe Hai Wenye Nyuso Nne” Ni Nani?
Yehova alimpa Ezekieli maono yanayotusaidia kuelewa mambo halisi ambayo hatungeweza kamwe kuyaelewa.

