Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!

Kitabu cha Ezekieli kina unabii mwingi unaokazia kurudishwa kwa ibada safi. Unabii huo unatuhusuje?

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Tunatumaini kwamba kitabu hiki kitakusaidia kumpa Yehova ibada safi ambayo anastahili kabisa kupokea.

Ufafanuzi wa Sehemu za Pekee

Masanduku ya kufundishia na mfuatano wa matukio unatupatia habari zaidi zinatakazotusaidia kuelewa kwa undani.

SURA YA 1

“Yehova Mungu Wako Ndiye Unayepaswa Kumwabudu”

Alipoanzisha uasi katika Edeni, Shetani hakushambulia tu haki ya Yehova Mungu ya kutawala, bali pia alishambulia ibada safi.

SURA YA 2

“Mungu Alikubali” Zawadi Zao

Kielelezo kilichowekwa na watu wenye imani kinafunua kwamba ibada inayokubalika inatia ndani mambo manne.

SURA YA 3

“Nikaanza Kuona Maono ya Mungu”

Maono ya kwanza ya Ezekieli yalimfanya alemewe kabisa. Mambo aliyoona yana maana kubwa kwa watumishi wa Mungu leo.

SURA YA 4

“Viumbe Hai Wenye Nyuso Nne” Ni Nani?

Yehova alimpa Ezekieli maono yanayotusaidia kuelewa mambo halisi ambayo hatungeweza kamwe kuyaelewa.

SURA YA 5

‘Ona Mambo Maovu na Yenye Kuchukiza Wanayofanya’

Ezekieli anaona mambo yenye kushtua ambayo yanaonyesha jinsi taifa lote lilivyopotoka kiroho.

SURA YA 6

“Sasa Mwisho Umekufikia”

Maigizo ya kinabii ya Ezekieli yalitabiri hasira ya Yehova dhidi ya Yerusalemu.

SURA YA 7

Mataifa Yatalazimika “Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova”

Mataifa yaliyolichafua jina la Mungu na kuwatesa au kuwapotosha watu wake hayangeepuka matokeo ya matendo yao. Tunajifunza nini kutokana na jinsi Waisraeli walivyoshughulika na mataifa hayo?

SURA YA 8

“Nitamweka Mchungaji Mmoja”

Mungu amwongoza Ezekieli aandike unabii kumhusu Masihi, Mtawala na Mchungaji wa wakati ujao wa watu wa Yehova, ambaye atarudisha ibada safi itakayodumu.

SURA YA 9

“Nitawapa Moyo Wenye Umoja”

Unabii uliotolewa kwa wahamishwa waaminifu Wayahudi huko Babiloni una maana gani kwetu?

SURA YA 10

“Mtakuwa Hai”

Ezekieli anaona maono ya bonde lililojaa mifupa mikavu ambayo inakuwa hai. Inamaanisha nini?

SURA YA 11

“Nimekuweka Kuwa Mlinzi”

Mlinzi huyu ana jukumu na wajibu gani? Anatoa onyo gani?

SURA YA 12

“Nitawafanya Kuwa Taifa Moja”

Yehova aahidi kuwaunganisha watu wake.

SURA YA 13

“Waeleze . . . Kuhusu Hekalu”

Ni nini maana ya hekalu ambalo Ezekieli aliona?

SURA YA 14

“Hii Ndiyo Sheria ya Hekalu”

Wayahudi walijifunza mambo gani kutokana na hekalu aliloona Ezekieli? Maono hayo yanatufundisha nini leo?

SURA YA 15

“Nitakomesha Ukahaba Wako”

Tunaweza kujifunza nini kutokana na ufafanuzi wa makahaba katika Ezekieli na Ufunuo?

SURA YA 16

“Uyatie Alama Mapaji ya Nyuso”

Katika siku za Ezekieli, watu waaminifu walitiwa alama ya kuokoka, hilo linatuhusuje leo?

SURA YA 17

“Niko Dhidi Yako, Ewe Gogu”

Gogu wa Magogu ni nani, na anashambulia nchi gani?

SURA YA 18

“Ghadhabu Yangu Kali Itawaka”

Shambulizi la Gogu lafanya Yehova akasirike, na kumfanya Mungu awalinde watu wake.

SURA YA 19

“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”

Kwa nini tunaweza kusema kwamba maono ya Ezekieli kuhusu mto unaotiririka kutoka hekaluni yalitimizwa, yanaendelea kutimizwa, na yataendelea kutimizwa wakati ujao?

SURA YA 20

‘Mtaigawa Nchi Iwe Urithi’

Katika maono, Mungu anamwagiza Ezekieli na wahamishwa wenzake waigawe Nchi ya Ahadi kati ya makabila ya Israeli.

SURA YA 21

“Jina la Jiji Hilo . . . Litakuwa, Yehova Yupo Hapo”

Tunapata masomo gani kutokana na maono ya Ezekieli kuhusu jiji na jina lake lenye maana?

SURA YA 22

“Mwabudu Mungu”

Kitabu hiki kimekusudiwa kuimarisha azimio letu la kumwabudu Yehova peke yake.

Muhtasari wa Ufafanuzi Mpya

Kwa nini baadhi ya uelewaji wetu wa unabii wa Ezekieli umebadilika?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 1A

Ibada Ni Nini?

Ibada ni nini hasa? Kitabu cha Ezekieli kinazungumziaje ibada? Ibada safi inahusisha nini?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 1B

Muhtasari wa Ezekieli

Kitabu hiki kinaweza kupangwa kulingana na mfuatano wa matukio na habari kuu.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 2A

Kuuelewa Unabii wa Ezekieli

Kitabu hiki kina maono, mifano, na vielezi. Huo ulikuwa ujumbe ulioongozwa na Mungu kuhusu mambo yatakayokuja.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 2B

Ezekieli​—Maisha na Nyakati Zake

Kulikuwa na manabii wengine kipindi cha Ezekieli. Katika siku zake kulikuwa na matukio muhimu katika historia ya watu wake.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 3A

Safari Ndefu ya Kwenda Babilonia

Inawezekana wahamishwa walitumia njia gani kutoka Yuda kwenda Babiloni?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 4A

‘Niliendelea Kuwatazama Viumbe Hai’

Kuna tofauti gani kati ya viumbe wanne ambao Ezekieli aliona katika maono na sanamu kubwa zilizokuwa katika nchi za Ashuru na Babiloni za kale?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA 5A

“Mwana wa Binadamu, Je, Unaona Hili?”

Ezekieli anaona mambo manne yenye kuchukiza katika hekalu na ua.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 6A

“Nyoa Kichwa Chako na Ndevu Zako”

Akiongozwa na Mungu, Ezekieli anaigiza maono ya kinabii ili kuonyesha jambo litakalotokea hivi karibuni huko Yerusalemu.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 7A

Mataifa Yaliyozunguka Yerusalemu

Yuda na mataifa jirani yalihusika katika vita.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 7B

Maneno Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli

Baadhi ya maneno yanatajwa mara nyingi katika kitabu hiki cha unabii.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 8A

Unabii Kumhusu Masihi​—Mwerezi Mkubwa

Ni nini maana ya fumbo lililo kwenye Ezekieli sura ya 17?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 8B

Unabii Kumhusu Masihi

Ezekieli atabiri kwamba tunapaswa kuwa na imani katika kiongozi wa wakati ujao wa watu wa Mungu.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 9A

Yehova Hutimiza Ahadi Zake​—Nyakati za Kale

Mungu amwongoza Ezekieli atangaze ahadi tano kuhusu kuwekwa huru na kurudishwa.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 9B

Kwa Nini 1919?

Kwa nini tunasema kwamba watu wa Mungu waliwekwa huru kutoka kwa utekwa wa Babiloni Mkubwa mwaka wa 1919?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 9C

Yehova Hutimiza Ahadi Zake​—Nyakati za Sasa

Baadhi ya ahadi za Mungu zimetimizwaje mara mbili?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 9D

Unabii Kuhusu Utekwa na Kurudishwa

Unabii kuhusu utekwa wa Wayahudi katika Babiloni la kale na kurudishwa ulitimizwa kwa njia kubwa zaidi kutaniko la Kikristo lilipokuwa mateka katika Babiloni la Kale na baadaye kurudishwa.

SANDUKU KUFUNDISHIA LA 9E

“Nyakati za Kurudishwa kwa Mambo Yote”

Mtume Petro aliongozwa kutabiri kipindi ambacho kingeanza na Kristo kuwa mfalme na kingeendelea mpaka mwisho wa miaka elfu moja.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10A

Ibada Safi​—Yarudishwa Hatua kwa Hatua

Ni mambo gani yaliyofanya kazi ya kuhubiri inayofanywa sasa iwezekane?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10B

Kuna Uhusiano Gani Kati ya “Mifupa Mikavu” na ‘Mashahidi Wawili’?

Unabii huu umetimizwaje katika nyakati zetu?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10C

Msaada wa Kusimama Tena

Huenda nyakati nyingine tukalemewa na kuchoka, lakini tunaimarishwa na maono ya mifupa mikavu iliyokuwa hai tena.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 11A

Baadhi ya Walinzi Walioweka Mfano Mzuri

Walikabili upinzani, walikuwa washikamanifu, na walitangaza maonyo na pia habari njema.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 12A

Kuunganishwa kwa Vijiti Viwili

Vijiti hivyo viliwakilisha nani, zamani na leo?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 13A

Mahekalu Tofauti, Masomo Tofauti

Kuna tofauti gani kati ya hekalu aliloona Ezekieli na hekalu la kiroho linalofafanuliwa na Paulo?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 14A

Masomo Kutokana na Hekalu Aliloona Ezekieli

Unapotazama mchoro wa hekalu la Ezekieli, ungependa kutumia mambo gani katika ibada yako?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 15A

Dada Waliokuwa Makahaba

Yehova anapotumia mfano wa Ohola na Oholiba anaonyesha jinsi anavyohisi kuhusu wale wanaolichafua jina lake takatifu na viwango vyake vya ibada safi.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 16A

Je, Yerusalemu Linawakilisha Dini Zinazodai Kuwa za Kikristo?

Kwa nini tulirekebisha uelewaji wetu?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 16B

Kulia kwa Uchungu na kwa Maumivu Makali, Kutiwa Alama, Kuponda​—Lini na Jinsi Gani?

Maono yaliyoandikwa kwenye Ezekieli sura ya 9 yanaweza kutusaidia kukabiliana na mwisho wa mfumo huu wa mambo tukiwa na uhakika.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 18A

Yehova Aonya Kuhusu Vita Vikubwa Vinavyokaribia

Biblia inatabiri kuhusu vita vikubwa vya mwisho ambapo Mungu atawaangamiza wote wanaompinga.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 19A

Mito ya Baraka Kutoka kwa Yehova

Baadhi ya waandikaji wa Biblia wametumia mfano huo kuonyesha baraka za Yehova.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 19B

Kijito Kinakuwa Mto Mkubwa!

Kijito kinachotiririka kutoka hekaluni kinamaanisha nini?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 20A

Kuigawa Nchi

Maono ya Ezekieli kuhusu kuigawa nchi hayakuwatia moyo tu Wayahudi waliohamishwa huko Babiloni bali pia watu wa Mungu leo.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 21A

“Mchango Mtakaoweka Kando”

Sehemu ambayo Mungu aliweka kando ilikuwa na maeneo gani matano? Yanatimiza kusudi gani?

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 22A

Kukabili Jaribu la Mwisho

Wale watakaoshinda jaribu la mwisho watapata nini?