MNARA WA MLINZI—TOLEO LA FUNZO Mei 2014

Toleo hili linazungumzia njia tatu tunazoweza kutumia katika huduma yetu kutoa majibu yenye kusadikisha tunapoulizwa maswali magumu. Kwa nini ni muhimu kwetu kuendelea kuwa washikamanifu kwa tengenezo la Mungu?

‘Chakula Changu Ni Kufanya Mapenzi ya Mungu’

Mfalme Daudi, mtume Paulo, na Yesu Kristo walifurahia kufanya mapenzi ya Mungu. Tutadumishaje au kuchochea upya bidii yetu tunapohubiri katika maeneo magumu?

Tunapaswa “Kumjibu Kila Mtu” Jinsi Gani?

Tunawezaje kutumia Maandiko kujadiliana kwa ustadi tunapoulizwa maswali magumu? Chunguza njia tatu tunazoweza kutumia kutoa majibu yenye kusadikisha.

Tumia Ile Kanuni Bora Katika Huduma Yako

Tunapaswa kumtendeaje kila mtu tunayekutana naye katika huduma yetu? Maneno ya Yesu katika Mathayo 7:12 yanahusuje kazi yetu ya kuhubiri?

SIMULIZI LA MAISHA

Yehova Amenisaidia Kwelikweli

Kenneth Little anaeleza jinsi ambavyo Yehova Mungu amemsaidia kushinda hali ya kuwa na wasiwasi na kuona haya. Ona jinsi Mungu alivyobariki jitihada zake maishani.

Yehova Ni Mungu Mwenye Utaratibu

Masimulizi kuhusu taifa la kale la Israeli na Wakristo wa karne ya kwanza yanaonyeshaje kwamba watumishi wa Yehova duniani wanapaswa kupangwa kitengenezo leo?

Je, Unasonga Mbele Pamoja na Tengenezo la Yehova?

Mfumo wa mambo wa Shetani utakomeshwa hivi karibuni. Kwa nini ni muhimu kwetu kuendelea kuwa washikamanifu kwa tengenezo ambalo Mungu anatumia duniani leo?

HIFADHI YETU YA VITU VYA KALE

“Kuna Kazi Zaidi ya Mavuno Inayopaswa Kufanywa”

Kuna Mashahidi wa Yehova zaidi ya 760,000 wanaoeneza kweli ya Biblia nchini Brazili. Kazi ya kuhubiri ilianzaje huko Amerika ya Kusini?