Yoeli 3:1-21
3 “Kwa maana, tazama! siku hizo na wakati huo,+ nitakapowarudisha mateka wa Yuda na Yerusalemu,+
2 mimi pia nitayakusanya pamoja mataifa yote+ na kuwaleta kwenye bonde la Yehoshafati;+ nami huko nitajiweka katika hukumu nao kwa sababu ya watu wangu na urithi wangu Israeli,+ ambao wamewatawanya katikati ya mataifa; nao waligawanya nchi yangu mwenyewe.+
3 Nao waliwapigia kura watu wangu;+ nao walikuwa wakimtoa mtoto wa kiume ili kumpata kahaba,+ walimuuza mtoto wa kike wapate divai ili wanywe.
4 “Pia, mna nini nami, enyi Tiro na Sidoni+ pia nanyi maeneo ya Ufilisti?+ Je, hivyo ndivyo mnavyonitendea kwa kunipa thawabu? Na ikiwa mnanitendea hivyo, matendo yenu nitayalipa haraka, naam, upesi, juu ya vichwa vyenu.+
5 Kwa sababu ninyi mmechukua fedha yangu mwenyewe na dhahabu yangu,+ nanyi mmeleta vitu vyangu vilivyo vyema katika mahekalu yenu;+
6 na wana wa Yuda na wana wa Yerusalemu mmewauza+ kwa wana wa Wagiriki,+ kwa kusudi la kuwaondolea mbali kutoka eneo lao wenyewe;+
7 tazama, ninawaamsha waje kutoka mahali ambapo mmewauza,+ na matendo yenu nitayalipa juu ya vichwa vyenu wenyewe.+
8 Nami nitawauza wana wenu na binti zenu mikononi mwa wana wa Yuda,+ nao watawauza kwa watu wa Sheba,+ taifa lililo mbali;+ kwa maana Yehova amesema hayo.
9 “Tangazeni mambo haya kati ya mataifa,+ ‘Takaseni vita! Amsheni wanaume wenye nguvu!+ Waacheni wakaribie! Na waje, wanaume wote wa vita!+
10 Fueni majembe yenu yawe panga na miundu+ yenu iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme: “Mimi ni mwanamume mwenye nguvu.”+
11 Toeni msaada wenu na mje, enyi mataifa yote jirani,+ mkusanyike pamoja.’ ”+
Mahali pale, Ee Yehova, uwashushe watu wako wenye nguvu.+
12 “Mataifa na yaamshwe, yaje kwenye bonde la Yehoshafati;+ kwa maana hapo nitaketi ili kuhukumu mataifa yote yanayozunguka pande zote.+
13 “Tieni ndani mundu,+ kwa maana mavuno yameiva.+ Njooni, teremkeni, kwa maana shinikizo la divai limejaa.+ Mitungi ya shinikizo inafurika; kwa maana ubaya wao umekuwa mwingi.+
14 Umati, umati umo katika bonde la uamuzi,+ kwa maana siku ya Yehova iko karibu katika bonde la uamuzi.+
15 Jua na mwezi vitakuwa giza, na nyota zitaondoa mwangaza wake.+
16 Na kutoka Sayuni Yehova atanguruma, kutoka Yerusalemu atatoa sauti yake.+ Na mbingu na dunia zitatikisika;+ bali Yehova atakuwa kimbilio kwa watu wake,+ na ngome kwa wana wa Israeli.+
17 Nanyi mtajua ya kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu,+ anayekaa katika Sayuni, mlima wangu mtakatifu.+ Na Yerusalemu litakuwa mahali patakatifu;+ wageni nao hawatapita tena kamwe kati yake.+
18 “Na itakuwa siku hiyo kwamba milima itatiririka divai tamu,+ na vilima vitatiririka maziwa, na sakafu za vijito vya Yuda zitatiririka maji. Na katika nyumba ya Yehova bubujiko litatoka,+ nalo litamwagilia maji bonde la mto la Mishita.+
19 Nayo Misri itakuwa mahame yenye ukiwa;+ nayo Edomu itakuwa nyika ya mahame yenye ukiwa,+ kwa sababu ya jeuri kwa wana wa Yuda, ambao walimwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao.+
20 Bali Yuda, itakaliwa sikuzote,+ na Yerusalemu kizazi baada ya kizazi.+
21 Na damu yao ambayo niliiona kuwa ina hatia nitaiona kuwa haina hatia;+ Yehova naye atakuwa anakaa katika Sayuni.”+

