Maombolezo 4:1-22
א [ʼAʹleph]
4 Lo! jinsi inavyofifia dhahabu yenye kung’aa, dhahabu iliyo nzuri!+Lo! jinsi mawe matakatifu+ yanavyomwagwa mbele ya barabara zote!+
ב [Behth]
2 Kwa habari ya wana wa Sayuni wenye thamani,+ waliopimwa uzito kwa kulinganishwa na dhahabu safi,Lo! jinsi wamehesabiwa kama mitungi mikubwa ya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!+
ג [Giʹmel]
3 Hata mbwa-mwitu wametoa maziwa. Wamenyonyesha watoto wao.Binti ya watu wangu anakuwa mkatili,+ kama mbuni nyikani.+
ד [Daʹleth]
4 Ulimi wa mtoto anayenyonya umekwama kwenye kaakaa lake kwa sababu ya kiu.+Watoto wameomba mkate.+ Hakuna anayewapa mkate huo.+
ה [Heʼ]
5 Wale waliokuwa wakila vitu vyenye kupendeza wameshikwa na mshangao barabarani.+Wale waliokuwa wakilelewa katika nguo nyekundu+ wamekumbatia marundo ya majivu.+
ו [Waw]
6 Adhabu kwa kosa la binti ya watu wangu pia inakuwa kubwa kuliko adhabu kwa kosa la dhambi ya Sodoma,+Lililoangamizwa kama kwa dakika moja, na ambalo hakuna mikono iliyojitokeza kulisaidia.+
ז [Zaʹyin]
7 Wanadhiri+ wake walikuwa safi kuliko theluji;+ walikuwa weupe kuliko maziwa.Kwa kweli walikuwa wekundu+ kuliko marijani; kung’arishwa kwao kulikuwa kama yakuti.+
ח [Chehth]
8 Sura yao imekuwa nyeusi kuliko weusi wenyewe. Hawakutambuliwa barabarani.+Ngozi yao imekauka juu ya mifupa yao.+ Imekauka kama mti.
ט [Tehth]
9 Wale waliouawa kwa upanga+ wamekuwa bora kuliko wale waliouawa kwa njaa,+Kwa sababu hao hudhoofika, wakichomwa kwa sababu ya ukosefu wa mazao ya shambani.
י [Yohdh]
10 Mikono ya wanawake wenye huruma imetokosa watoto wao wenyewe.+Wamekuwa kama mkate wa kufariji mtu wakati wa kuvunjika kwa binti ya watu wangu.+
כ [Kaph]
11 Yehova ametimiza ghadhabu yake.+ Amemwaga hasira yake inayowaka.+Naye anawasha moto katika Sayuni, unaoteketeza misingi yake.+
ל [Laʹmedh]
12 Wafalme wa dunia na wakaaji wote wa nchi yenye kuzaa hawakuwa wameamini+Kwamba mpinzani na adui wataingia katika malango ya Yerusalemu.+
מ [Mem]
13 Kwa sababu ya dhambi za manabii wake, makosa ya makuhani wake,+Mlikuwa katikati yake wale wanaomwaga damu ya waadilifu.+
נ [Nun]
14 Wametanga-tanga kama vipofu+ barabarani.+ Wamechafuliwa na damu,+Hivi kwamba hakuna wanaoweza kugusa mavazi yao.+
ס [Saʹmekh]
15 “Ondokeni njiani! Najisi!”+ Wamewapaazia sauti. “Ondokeni njiani! Ondokeni njiani! Msiguse!”+Kwa maana wamekosa makao.+ Pia wametanga-tanga.+ Watu wamesema kati ya mataifa: “Hawatakaa tena kama wageni.+
פ [Peʼ]
16 Uso wa Yehova umewatawanya.+ Hatawatazama tena.+Watu hawataonyesha kujali hata kwa walio makuhani.+ Hakika hawatawakubali hata walio wanaume wazee.”+
ע [ʽAʹyin]
17 Tukiwa tungali bado tunaishi, macho yetu huendelea kudhoofika bure kwa kutazamia msaada wetu.+Wakati wa kutazama kwetu tumetazamia taifa ambalo haliwezi kuleta wokovu.+
צ [Tsa·dhehʹ]
18 Wamewinda hatua zetu+ hivi kwamba hakuna kutembea katika viwanja vyetu vya watu wote.Mwisho wetu umekaribia. Siku zetu zimetimia, kwa maana mwisho wetu umekuja.+
ק [Qohph]
19 Wenye kutufuatilia wamekuwa wepesi kuliko tai wa mbinguni.+Wametufuatilia vikali juu ya milima.+ Wametuvizia nyikani.+
ר [Rehsh]
20 Pumzi ya mianzi ya pua zetu,+ mtiwa-mafuta wa Yehova,+ amenaswa katika shimo lao kubwa,+Yule ambaye tumesema habari zake: “Tutaishi chini ya kivuli+ chake kati ya mataifa.”+
ש [Sin]
21 Furahi na kushangilia,+ Ee binti Edomu,+ wewe unayekaa katika nchi ya Usi.+Kwako wewe pia kikombe kitapita.+ Utalewa na kujionyesha ukiwa uchi.+
ת [Taw]
22 Kosa lako, Ee binti Sayuni, limefikia mwisho wake.+ Hatakupeleka tena uhamishoni.+Amegeuza fikira zake kwa kosa lako, Ee binti Edomu. Amefunua dhambi zako.+

