Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | SABABU GANI YESU ALITESEKA NA KUFA?

Mambo Hayo Yalitokea Kabisa?

Mambo Hayo Yalitokea Kabisa?

Katika mwaka wa 33, Yesu wa Nazarethi aliuawa. Alishitakiwa kwa uongo kama anachochea watu kupinga serikali, alipigwa kama nyama, na kutundikwa kwenye muti. Alikufa katika maumivu makali sana. Lakini Mungu alimufufua, na kisha siku 40, alipanda mbinguni.

Habari hiyo ya pekee inazungumuziwa katika vitabu ine vya Injili vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, yenye watu wengi wanaita Agano Jipya. Mambo hayo yalitokea kabisa? Hilo ni ulizo nzito, pia lenye kufaa. Kama mambo hayo hayakutokea, imani ya Wakristo haina faida na tumaini la uzima wa milele katika Paradiso ni ndoto tu. (1 Wakorintho 15:14) Lakini kama mambo hayo yalitokea kabisa, wanadamu wako na tumaini la muzuri juu ya wakati unaokuja; wewe pia unaweza kuishi wakati huo. Kwa hiyo, habari za vitabu vya Injili ni za kweli ao ni za kuwazia tu?

MAMBO YA HAKIKA YANAONYESHA NINI?

Tofauti na habari za kuwazia, maandishi ya vitabu vya Injili yanaeleza habari za kweli kabisa na hata mambo madogo-madogo. Kwa mufano, maandishi hayo ya Injili yanajaa majina ya nafasi za kweli, na nafasi nyingi kati ya hizo zinaweza kutembelewa leo. Yanazungumuzia watu wa kweli, na wanahistoria wa ulimwengu wanahakikisha kama watu hao waliishi.—Luka 3:1, 2, 23.

Yesu mwenyewe anazungumuziwa na waandikaji wa ulimwengu wa mwaka kati ya 1 na 200. * Namna Yesu aliuawa, kama vile inaonyeshwa katika vitabu vya Injili, inapatana na namna Waroma walikuwa wanaua watu wakati huo. Tena, mambo yenye yalitokea yanaelezwa kwa uaminifu na kwa ukweli; hata makosa ya wanafunzi fulani wa Yesu yanaonyeshwa. (Mathayo 26:56; Luka 22:24-26; Yohana 18:10, 11) Mambo hayo yote yanaonyesha kabisa kama waandikaji wa vitabu vya Injili walikuwa waaminifu na hawakukosea kuhusu mambo waliandika juu ya Yesu.

TUSEME NINI JUU YA UFUFUO WA YESU?

Hata kama watu wengi wanaitika kuwa Yesu aliishi na alikufa, wengine wanaweza kuwa na mashaka juu ya ufufuo wake. Hata mitume wake hawakuamini wakati waliambiwa kwa mara ya kwanza kama Yesu alifufuka. (Luka 24:11) Lakini, mashaka yote yaliisha wakati watu fulani na wanafunzi wengine walimuona kwa wakati mbalimbali Yesu mwenye alikuwa amefufuliwa. Kwa kweli, wakati fulani kulikuwa watu zaidi ya 500 wenye walimuona.—1 Wakorintho 15:6.

Hata kama wanafunzi wa Yesu walikuwa katika hatari ya kufungwa na kuuawa, walitangaza kwa ujasiri ufufuo wa Yesu kwa watu wote, na kwa wenye walimuua. (Matendo 4:1-3, 10, 19, 20; 5:27-32) Wanafunzi hao wengi wangekuwa na ujasiri ikiwa hawakukuwa hakika kama Yesu alifufuliwa kabisa? Kusema kweli, ufufuo wa Yesu ulitokea kabisa, hilo ndilo jambo lenye lilifanya Ukristo ukuwe na matokeo makubwa wakati huo na hata leo.

Habari za vitabu vya Injili kuhusu kifo cha Yesu na ufufuo wake ziko na ushuhuda wote wenye kuonyesha kama ni habari za kihistoria za kweli kabisa. Kusoma kwa uangalifu habari hizo, kutakuhakikishia kama mambo hayo yalitokea kabisa. Tena, utakuwa hakika zaidi wakati unaelewa sababu gani mambo hayo yalitokea. Habari yenye kufuata itazungumuzia jambo hilo.

^ fu. 7 Tasito, mwenye alizaliwa mwaka wa 55 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, aliandika kama “Kristo, mwenye jina [Wakristo] lilitokana na jina lake, aliuawa katika mikono ya Pontio Pilato, mumoja kati ya magavana wetu, wakati wa utawala wa Tiberio.” Yesu anatajwa tena na mwanahistoria Suetonius (mwenye alizaliwa katika mwaka wa 69); mwanahistoria Muyahudi Joseph (mwenye alizaliwa katika mwaka wa 37 ao 38); na Plini Mudogo, gavana wa Bithinia (mwenye alizaliwa katika mwaka wa 61 ao 62).