Kiswahili
“Mwenye Hekima Moyoni”
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1102002040/univ/art/1102002040_univ_sqr_xl.jpg
cl uku. 201

SEHEMU YA 3

“Mwenye Hekima Moyoni”

“Mwenye Hekima Moyoni”

Hekima ya kweli ni mojawapo ya mambo yenye thamani sana unayoweza kutafuta. Yehova peke yake ndiye Chanzo cha hekima hiyo. Katika sehemu hii, tutachunguza kwa undani hekima ya Yehova Mungu isiyo na mipaka. Mwanamume mwaminifu Ayubu alisema hivi kumhusu: “Yeye ni mwenye hekima moyoni.”​—Ayubu 9:4.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 17

“Lo! Jinsi kilivyo kina cha . . . Hekima ya Mungu!”

Kwa nini hekima ya Mungu ni bora kuliko ujuzi, uelewaji, na utambuzi wake?

SURA YA 18

Hekima ya “Neno la Mungu”

Kwa nini Mungu aliwatumia wanadamu kuandika mawazo yake katika kitabu, na kwa nini baadhi ya mambo yanazungumziwa na mengine hayazungumziwi katika kitabu hicho?

SURA YA 19

“Hekima ya Mungu katika Siri Takatifu”

Ni siri gani takatifu ambayo Mungu ameifunua hatua kwa hatua?

SURA YA 20

“Mwenye Hekima Moyoni”​—Lakini Mnyenyekevu

Bwana Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote mzima anawezaje kuwa mnyenyekevu?

SURA YA 21

Yesu Afunua “Hekima Kutoka kwa Mungu”

Mafundisho ya Yesu yalikuwa yenye kuvutia sana hivi kwamba katika pindi moja maofisa waliotumwa ili kumkamata walirudi mikono mitupu!

SURA YA 22

Je, “Hekima Inayotoka Juu” Inafanya Kazi Maishani Mwako?

Biblia ina njia nne za kukusaidia kukuza hekima ya kimungu.