“Njoo Uwe Mfuasi Wangu”
Kusudi la kitabu hiki si kutupatia kikamili muhtasari wa maisha na huduma ya Yesu, bali ni kutusaidia kuona vizuri zaidi jinsi tunavyoweza kumfuata.
Utangulizi
Upendo wako kwa Yesu na uendelee kukua na uendelee kumfuata kwa ukaribu ili uufurahishe moyo wa Yehova sasa na milele.
SURA YA 1
“Uwe Mfuasi Wangu”—Yesu alimaanisha nini?
Kuwa mfuasi wa kweli wa Yesu kunahusisha mengi zaidi tu ya maneno na hisia.
SURA YA 2
“Njia na Kweli na Uzima”
Ili kumfikia Baba ni lazima tupitie kwa Mwana. Yesu amepewa jukumu muhimu katika kutimizwa kwa kusudi la Mungu.
SEHEMU YA 1
‘Njoo Umwone’ Kristo
SURA YA 3
“Mimi Ni . . . Mnyenyekevu Moyoni”
Yesu alionyesha unyenyekevu kuanzia mwanzo hadi mwisho wa huduma yake hapa duniani.
SURA YA 4
“Tazama! Simba wa Kabila la Yuda”
Yesu alionyesha ujasiri kama wa simba katika njia tatu: kwa kuitetea kweli, kutetea haki, na kukabili upinzani.
SURA YA 6
“Alijifunza Kutii”
Kwa kuwa Yesu alimtii Baba yake sikuzote, kwa nini tunaweza kusema kwamba “alijifunza kutii” na alifanywa “kuwa mkamilifu”?
SURA YA 7
“Mfikirieni Sana Yule Ambaye Amevumilia”
Yesu alivumilia kikamili. Ni nini kilichomsaidia kuvumilia? Tunawezaje kufuata mfano wake wa uvumilivu?
SEHEMU YA 2
‘Kufundisha na Kuhubiri Habari Njema.’
SURA YA 8
“Nilitumwa Kufanya Hivyo”
Chunguza ni kwa nini Yesu alihubiri, habari alizohubiri, na mtazamo aliokuwa nao kuhusu mgawo wake akiwa hapa duniani.
SURA YA 9
“Nendeni Mkafanye Wanafunzi”
Mtu anaweza kuwa mfuasi wa kweli wa Kristo, kwa kufuata amri ya Yesu ya kufanya wanafunzi.
SURA YA 10
“Imeandikwa”
Kunukuu Neno la Mungu, kulitetea, na kulifafanua ni kati ya njia kuu za kuiga ustadi wa Yesu wa kuwafundisha wengine kweli.
SURA YA 11
“Hakuna mtu mwingine yeyote ambaye amewahi kuzungumza hivyo.”
Chunguza njia tatu za Yesu ambazo alitumia kufundisha na jinsi tunavyoweza kuzitumia.
SURA YA 12
“Hakuwa Akizungumza Nao Bila Mfano”
Biblia inatupatia sababu mbili muhimu zilizomfanya Yesu atumie mifano.
SEHEMU YA 3
“Upendo Alio Nao Kristo Hutuchochea”
SURA YA 14
“Umati Mkubwa Ukamjia”
Watu wengi kutia ndani watoto hawakusita kumkaribia Yesu. Ni nini kilichomfanya Yesu awe mwenye kufikika?
SURA YA 15
“Akawasikitikia”
Kwa nini ni muhimu kufuata mfano wa Yesu katika kuwaonyesha wengine rehema na huruma?
SURA YA 16
“Yesu . . . Aliwapenda Mpaka Mwisho”
Katika huduma yake yote, Yesu aliwaonyesha wanafunzi wake kwamba anawapenda. Tunawezaje kuiga upendo huo tunaposhughulika na wengine?
SURA YA 17
“Hakuna Mtu Aliye na Upendo Mkuu Kuliko Huu”
Tunawezaje kufuata mfano wa Yesu wa kuwa na upendo wa kujidhabihu?
SURA YA 18
“Endelea Kunifuata”
Ikiwa tutaendelea kumfuata Yesu siku baada ya siku, tunaweza kufurahia kuwa na dhamiri safi na tumaini zuri la wakati ujao.

