DESEMBA 22, 2021
FILIPINO
Kimbunga Rai Chaipiga Filipino
Desemba 16 hadi 18, 2021, Kimbunga Rai (kinachojulikana nchini Filipino kama Odette) kilipiga maeneo mbalimbali ya Filipino. Kilipopiga kwa mara ya kwanza katika Kisiwa cha Siargao, Filipino, kilikuwa na upepo wenye kuendelea uliovuma kwa kilomita 195 kwa saa. Mikoa ya Mindano Kaskazini, Luzon Kusini, na Visayas vilikabili uharibifu mkubwa.
Athari kwa Ndugu na Dada Zetu
Kwa kusikitisha, wahubiri 4 walikufa
Mhubiri mmoja bado hajulikani alipo
Ndugu na dada 12 walijeruhiwa
Zaidi ya wahubiri 2,000 wamelazimika kuhama makazi yao
Nyumba 246 ziliharibiwa kabisa
Nyumba 327 zilipata uharibifu mkubwa
Nyumba 1,174 zilipata uharibifu mdogo
Majumba 43 ya Ufalme yalipata uharibifu mdogo
Jitihada za Kutoa Msaada
Halmashauri 6 za Kutoa Msaada zimeanzishwa ili kusimamia kazi ya kutoa msaada
Wazee wa eneo hilo wanawafanyia ziara za uchungaji wale walioathiriwa, kutia ndani wale waliowapoteza wapendwa wao
Jitihada zote za kutoa msaada zinafanywa kulingana na miongozo ya usalama ya kujilinda dhidi ya COVID-19
Chini ya mwongozo wa wazee, ndugu na dada katika maeneo ambayo hayakuathiriwa walitoa chakula na mavazi kwa ajili ya wahubiri walioathiriwa na kimbunga hicho. Vifurushi vya chakula kutoka Jiji la Davao vilisambazwa mara moja kwa familia zilizokuwa na uhitaji katika Jiji la Surigao.
Tunasikitika kusikia kwamba baadhi ya ndugu na dada zetu wapendwa walikufa katika janga hilo. Tunapoendelea kuvumilia “nyakati [hizi] za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,” na tuendelee kumtegemea Yehova ili atupe faraja na kutuimarisha.—2 Timotheo 3:1.

