Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Sababu gani Biblia iko na unabii mbalimbali?

Sababu gani Biblia inaeleza mambo yenye kutokea leo?—Luka 21:10, 11.

Unabii mbalimbali wenye mafasirio mengi unapatikana katika Biblia. Hakuna mutu anaweza kutabiri wakati unaokuja kwa kutoa mafasirio mengi. Kwa hiyo, kutimizwa kwa unabii mbalimbali wa Biblia kunatupatia uhakika kama Biblia ni Neno la Mungu.—Soma Yoshua 23:14; 2 Petro 1:20, 21.

Unabii mbalimbali wa Biblia wenye umekwisha kutimia unatupatia sababu ya muzuri ya kuamini Mungu. (Waebrania 11:1) Tena, unatupatia uhakika wa kwamba ahadi za Mungu juu ya wakati muzuri unaokuja zitatimia. Kwa hiyo, unabii wa Biblia unatupatia tumaini lenye kuwa hakika.—Soma Zaburi 37:29; Waroma 15:4.

Unabii mbalimbali wa Biblia unatusaidia namna gani?

Unabii fulani unaambia watumishi wa Mungu watende jambo fulani. Kwa mufano, wakati Wakristo wa kwanza waliona unabii fulani juu ya Yerusalemu unatimizwa, walitoka katika muji huo. Kisha, wakati muji huo uliharibiwa kwa sababu watu wengi walikataa Yesu, Wakristo walikuwa mbali katika nafasi salama.—Soma Luka 21:20-22.

Leo, unabii mbalimbali wenye umekwisha kutimia, unaonyesha kama hivi karibuni Ufalme wa Mungu utaharibisha serikali zote za wanadamu. (Danieli 2:44; Luka 21:31) Kwa hiyo, ni jambo la haraka kila mutu afanye nguvu sana ili akubaliwe na Yesu Kristo, Mufalme mwenye Mungu ameweka.—Soma Luka 21:34-36.