Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo Yenye Manabii Wanatufundisha Kumuhusu Mungu

Mambo Yenye Manabii Wanatufundisha Kumuhusu Mungu

Zamani, Mungu alipatia manabii wake ujumbe mbalimbali kwa ajili ya wanadamu. Ule ujumbe unaweza kutuonyesha namna ya kupata baraka ya Yehova? Ndiyo. Tuone mambo yenye tunajifunza kupitia manabii watatu waaminifu.

ABRAHAMU

Mungu hana ubaguzi na anapenda kubariki watu wote.

Mungu aliahidi nabii Abrahamu hivi: “Familia zote za dunia hakika zitabarikiwa kupitia wewe.”​—Mwanzo 12:3.

Ile inatufundisha nini? Mungu anatupenda sana na anapenda kubariki familia zote, ni kusema, wanaume, wanamuke, na watoto wote wenye wanamutii.

MUSA

Mungu ni mwenye rehema na anabariki wale wote wenye wanajikaza kumujua.

Mweza-Yote alipatia Musa uwezo wa kufanya miujiza ya ajabu. Ijapokuwa ile, Musa alisali: “Nijulishe njia zako, ili nikujue wewe na niendelee kukubaliwa mbele ya macho yako.” (Kutoka 33:13) Mungu alifurahia ombi la Musa na alimubariki kwa kumusaidia ajue na aelewe muzuri zaidi njia na sifa zake. Kwa mufano, Musa alijifunza kama Muumbaji ni “Mungu mwenye rehema na huruma.”​—Kutoka 34:6, 7.

Ile inatufundisha nini? Ikuwe tuko wanaume, wanamuke, ao watoto, Mungu anapenda kutubariki sisi wote kama tunajikaza kumujua muzuri. Anatuonyesha mu Maandiko Matakatifu namna ya kumuabudu na kama anapenda kutukubali na kutubariki.

YESU

Kwa huruma, Yesu aliponyesha aina zote za magonjwa

Tunaweza kupata baraka za milele za Mungu kama tunajifunza kumuhusu Yesu na kufanya mambo yenye alifanya na yenye alifundisha.

Neno la Mungu liko na habari mingi kuhusu maisha na mafundisho ya Yesu. Mungu alipatia Yesu uwezo wa kufanya miujiza mingi ya ajabu, kama vile kuponyesha vipofu, viziwi, na vilema. Alifufua hata wafu. Kwa kufanya vile, Yesu alionyesha baraka zenye Mungu ataletea wanadamu wote wakati wenye kuja. Alionyesha namna kila mutu anaweza kupata zile baraka kwa kusema: “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli, na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.”​—Yohana 17:3.

Yesu alikuwa mwema, mwenye huruma, na mupole. Wanaume na wanamuke, vijana na wazee, walikuja kwake kwa uwingi wakati aliwaambia: “Mujifunze kupitia mimi, kwa maana mimi ni mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo, na mutapata pumuziko kwa ajili yenu.” (Matayo 11:29) Tofauti na watu wengine wa wakati wake wenye walitendea mubaya wanamuke, Yesu alitendea wanamuke kwa wema, na aliwaheshimia.

Ile inatufundisha nini? Yesu alipenda sana watu, na alituachia mufano muzuri kuhusu namna tunapaswa kutendeana.

YESU HAIKO MUNGU

Maandiko Matakatifu inafundisha kama “kwa kweli kwetu sisi kuko Mungu mumoja” na kama Yesu Kristo ni mujumbe munyenyekevu wa Mungu. (1 Wakorinto 8:6) Yesu alisema waziwazi kama Mungu ni mukubwa kuliko yeye na kama Mungu alimutuma ku dunia.​—Yohana 11:41, 42; 14:28. *

^ fu. 17 Ili kujua mingi zaidi kumuhusu Yesu Kristo, ona sehemu ya 8 na 9 ya broshua Imani ya Kweli​—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha yenye kupatikana ku www.jw.org/sw.