Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaweza kusaidia wengine bila kuangalia miaka, inchi, ao dini yao?

Tunapaswa Kusaidia Wenye Wako na Lazima ya Musaada juu Tupate Baraka

Tunapaswa Kusaidia Wenye Wako na Lazima ya Musaada juu Tupate Baraka

Watu wengi mu dunia wako na lazima ya chakula na nyumba. Wamoja wako tu na lazima ya tumaini la wakati wenye kuja. Namna gani bidii yetu ya kusaidia wale watu inaweza kufanya Mungu atukubali na kutubariki?

MAMBO YENYE MAANDIKO MATAKATIFU INASEMA

“Mwenye anaonyesha mutu wa hali ya chini wema anamukopesha Yehova, na Yeye atamulipa kwa sababu ya mambo yenye anatenda.”​—MEZALI 19:17.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUSAIDIA MUTU MWENYE IKO NA LAZIMA YA MUSAADA?

Yesu alitoa mufano wa mwanaume mwenye alishambuliwa na wanyanganyi na wakamuacha karibu kufa. (Luka 10:29-37) Mutu fulani wa roho muzuri mwenye alikuwa hamujue alisimama na kusaidia ule mwanaume mwenye alikuwa ameumizwa mubaya. Alimusaidia hata kama hakukuwa wa kabila yake.

Ule mwanaume wa roho muzuri hakumutolea tu matunzo ya kwanza-kwanza na musaada wa kimwili lakini pia alimufariji na kumutuliza.

Ule mufano unatufundisha nini? Yesu alipenda kutufundisha kama tunapaswa kufanya yote yenye tunaweza ili kusaidia wale wenye wako na lazima ya musaada. (Mezali 14:31) Maandiko Matakatifu inafundisha kama hivi karibuni Mungu atamaliza umaskini na mateso. Lakini, tunaweza kujiuliza: Mungu atafanya vile namna gani na wakati gani? Habari yenye kufuata itazungumuzia baraka zenye Muumbaji wako mwenye upendo amekutayarishia.