Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unajua Wakati?

Unajua Wakati?

KAMA unapenda kujua wakati, unafanyaka nini? Inawezekana kabisa unaangaliaka ku saa yako. Kama rafiki anakuuliza ni saa ngapi, utamujibu namna gani? Kuko njia mbalimbali za kusema wakati. Ni njia gani?

Tuseme kama ni saa saba na dakika 30 kisha midi. Unaweza kumuambia kama ni saa 7:30. Kulingana na mahali kwenye unaishi na namna watu wanazoea kusema, unaweza kusema kama ni saa 7:30 (13:30). Njia hiyo ya kusema wakati inategemea ufundi wa kugawanya siku moja katika saa 24. Mahali pengine wakati huo unaweza hata kusemwa “saa munane kosa dakika 30,” ni kusema, kunakosa dakika 30 mbele ikuwe saa munane.

Juu uko musomaji wa Biblia, pengine unaweza kujiuliza namna gani watu walikuwa wanasema wakati katika kipindi Biblia iliandikwa. Kulikuwa njia mbalimbali za kusema wakati. Sehemu ya Biblia ya Maandiko ya Kiebrania inataja “asubui,” “muchana,” “katikati ya muchana,” na “mangaribi.” (Mwa. 8:11; 19:27; 43:16; Kum. 28:29; 1 Fa. 18:26) Lakini wakati fulani, Biblia inataja wakati kamili.

Katika kipindi Biblia iliandikwa, watu walizoea kutumikisha walinzi. Walinzi walikuwa wa lazima zaidi sana wakati wa usiku. Mamia ya miaka mbele Yesu azaliwe, Waisraeli waligawanya usiku katika vipindi tatu vyenye kuitwa makesha. (Zb. 63:6) Andiko la Waamuzi 7:19 linataja “kesha la katikati ya usiku.” Wakati wa Yesu, Wayahudi walitumia njia ya Wagiriki na Waroma ya kugawanya usiku katika vipindi ine vya makesha.

Vitabu vya Injili vinazungumuzia mara nyingi makesha hayo. Kwa mufano, wakati Yesu alitembea juu ya maji kusudi aende kwenye mashua mahali wanafunzi wake walikuwa, ilikuwa “katika kesha la ine (4) la usiku.” (Mt. 14:25) Katika mufano moja, Yesu alisema hivi: “Kama mwenye nyumba angejua ni katika kesha gani mwizi atakuja, angekaa macho na hangeruhusu nyumba yake ivunjwe.”​—Mt. 24:43, maelezo ya chini.

Yesu alizungumuzia makesha hayo ine wakati aliambia wanafunzi hivi: “Muendelee kukesha, kwa maana hamujue bwana wa nyumba atakuja wakati gani, kama ni mangaribi, ao katikati ya usiku, ao mbele ya mapambazuko, ao asubui sana.” (Mk. 13:35) Kesha la kwanza kati ya makesha hayo, ni “mangaribi,” lilianza wakati jua lilishuka mupaka saa 3 hivi ya usiku. Kesha la pili, ni “katikati ya usiku,” lilianza saa 3 hivi ya usiku mupaka katikati ya usiku. Kesha la tatu, lenye kuitwa “mbele ya mapambazuko,” ao “wakati jogoo anawika,” lilianza katikati ya usiku mupaka saa 9 hivi ya asubui. Katika usiku wenye Yesu alikamatwa, inawezekana jogoo aliwika kabisa katika kesho hilo. (Mk. 14:72) Kipindi cha ine cha usiku, ni kesha la “asubui sana,” kilianza saa 9 hivi mupaka asubui wakati jua linatokea.

Kwa hiyo, hata kama katika kipindi Biblia iliandikwa, watu hawakukuwa na vyombo vya kuonyesha saa, walikuwa na njia ya kusema wakati wa muchana ao wa usiku.