Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA

Biblia Ni ya Maana Leo?

Biblia Ni ya Maana Leo?

‘Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilipata furaha’

HILTON alipenda muchezo wa ngumi (boxe). Wakati alikuwa na miaka saba, alikuwa tayari ameanza kupigana, kwenye uwanja wa kupigania ngumi ao nafasi ingine! Wakati alikuwa kwenye masomo ya sekondari alikuwa anazunguka-zunguka pembeni ya marafiki wake ili kutafuta mutu wa kupiganisha. Anasema hivi: “Niliiba, nilicheza michezo ya feza, niliangalia ponografia, niliwasumbua wanawake, na niliwatukana wazazi wangu. Mwenendo wangu ulikuwa hivyo, na kwa sababu hiyo wazazi wangu waliwaza kuwa siwezi kubadilika. Kisha kumaliza masomo ya sekondari, niliondoka nyumbani.”

Wakati Hilton alirudia nyumbani kisha miaka 12, wazazi wake hawakuamini kwa vyepesi kuwa huyo alikuwa mutoto wao! Alikuwa mupole, mwenye kujizuia, na mwenye heshima. Ni nini kilimuchochea afanye mabadiliko hayo ya kushangaza? Wakati alikuwa mbali na wazazi wake, alianza kufikiri sana ikiwa maisha yake yalikuwa yanaelekea wapi. Alichunguza pia Biblia ili kuona ikiwa ingemusaidia kubadilisha maisha yake. Hilton anasema hivi: “Nilitenda kulingana na mambo nilisoma katika Biblia, hilo lilimaanisha kuacha mwenendo wangu wa zamani na kufuata amri ya kutii wazazi wangu inayopatikana katika andiko la Waefeso 6:2, 3. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilipata furaha ya kweli, na nilifurahisha baba na mama yangu kuliko kuwaumiza moyoni!”

Habari ya Hilton inakazia kuwa kanuni za Biblia ni za maana na zina uwezo wa kubadilisha maisha ya watu. (Waebrania 4:12) Acha tuzungumuzie kanuni fulani kati ya kanuni hizo, ni kusema, kufuatia haki, kujizuia, uaminifu, na upendo, na namna zinaweza kufanya maisha yetu yakuwe ya muzuri kabisa.