Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | BIBLIA NI YA MAANA LEO?

Kanuni Zinazotumika Sikuzote na Zenye Kufaa Kila Mutu—Kujizuia

Kanuni Zinazotumika Sikuzote na Zenye Kufaa Kila Mutu—Kujizuia

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mutu mujinga anaiachilia roho yake yote, lakini mwenye hekima anaituliza mupaka mwisho.’Methali 29:11.

“Ninajisikia kama vile nilifufuliwa kutoka kwa wafu!”

FAIDA: Ikiwa unaombwa kuandika faida zote za kujizuia, unaweza kuwa na lazima ya karatasi nyingi! Kwa kifupi, sifa hiyo inalinda afya yetu ya kimwili. Biblia inasema hivi: ‘Moyo mutulivu ni uzima wa mwili wenye nyama.’ Inasema pia kama “moyo wenye shangwe ni dawa nzuri.” (Methali 14:30; 17:22) Tofauti na hilo, uchunguzi mbalimbali unaonyesha kuwa kukasirika kwa vyepesi na chuki vinaongeza hatari ya kupata magonjwa, zaidi sana ugonjwa wa moyo. Kwa kweli, zaidi ya kusaidia mutu kuwa na afya ya muzuri, faida za kujizuia ni nyingi.

Cassius, aliye sasa na miaka kati ya 31 na 40, anasema hivi: “Nilikuwa mugomvi na mwenye hasira sana, na mara nyingi nilianzisha mapigano. Sikujiheshimia sana. Lakini mambo hayo yote yalibadilika wakati nilianza kutumikisha kanuni za Biblia. Nilijifunza kuzuia hasira yangu na kuonyesha unyenyekevu na roho ya kusamehe. Kama singefanya hivyo, ningeishia katika gereza. Kwa kweli, ninajisikia kama vile nilifufuliwa kutoka kwa wafu!”

Cassius alijifunza kuzuia hasira yake