Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA KUULIZA MAULIZO | GUILLERMO PEREZ

Muganga Anayepasua Watu Anaeleza Imani Yake

Muganga Anayepasua Watu Anaeleza Imani Yake

Muganga Guillermo Perez aliyekuwa kiongozi wa kupasua watu kwenye vitanda 700 vya hospitali ya Afrika ya Kusini aliachishwa kazi hivi karibuni kwa sababu ya uzee. Alikuwa anaamini mageuzi kwa miaka mingi. Lakini kisha, aliitika kwamba mwili wa mwanadamu uliumbwa na Mungu. Gazeti Amuka! lilimuuliza juu ya imani yake.

Tafazali, utuambie kwanza sababu gani hapo mbele uliamini mageuzi.

Hata ikiwa nilikuwa Mukatoliki nilipokomaa, nilikuwa na mashaka juu ya Mungu. Kwa mufano, singeweza kumuamini Mungu anayeunguza watu katika moto wa mateso. Kwa hiyo, wakati walimu wangu kwenye masomo ya juu walinifundisha kwamba vitu vilivyo na uzima vilijitokeza kupitia mageuzi na kwamba havikuumbwa na Mungu, nilikubaliana na mawazo hayo, nikifikiri kwamba kuna mambo yanayoyahakikisha. Kwa kweli, dini yangu haikukataa mageuzi lakini ilisema kwamba mageuzi yaliongozwa na Mungu.

Ni nini iliyofanya uanze kupendezwa na Biblia?

Bibi yangu, Susana, alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Walimuonyesha kupitia Biblia kwamba Mungu hawatese watu katika moto wa mateso. * Walimuonyesha pia kusudi la Mungu la kuifanya dunia kuwa paradiso. * Mwishowe, tulipata mafundisho yenye kupatana na akili! Katika mwaka wa 1989, Shahidi wa Yehova anayeitwa Nick alianza kunitembelea. Siku moja tulipozungumuza juu ya mwili wa mwanadamu na namna ulivyotokezwa, nilishangaa na mafasirio mepesi na yenye kupatana na akili ya maneno ya Biblia katika andiko la Waebrania 3:4 linalosema kwamba ‘Kila nyumba inajengwa na mutu fulani, lakini yeye aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.’

Kujifunza kwako mwili wa mwanadamu kulikusaidia uitike uumbaji?

Ndiyo. Namna mwili wetu unavyojitunza wenyewe iliumbwa kwa njia ya ajabu sana. Kwa mufano, matunzo ya kidonda yanaomba hatua ine zenye kufuatana, na hatua hizo zote zilinikumbusha kwamba nikiwa mupasuaji, nilitumika tu na namna mwili wetu umefanywa ili kujitunza wenyewe.

Tueleze, inakuwa namna gani wakati mwili wetu unaumia?

Katika sekunde chache, hatua ya kwanza ya mufuatano wa utendaji mbalimbali inaanza kutumika ili kuzuia mutiririko wa damu. Utendaji huo ni mugumu kueleweka na ni wenye matokeo. Ninaweza kuongezea kwamba, mufumo wetu wa kuzungusha damu katika mwili, ulio na kilometa 100000 hivi za mishipa ya damu, unapita uwezo wa mabomba yanayotengenezwa na mainjinia, kwa sababu una uwezo wa kuzuia kuvuja kwa damu na kujitunza yenyewe.

Ni mambo gani yanayofanywa katika hatua ya pili ya kujitunza kwa mwili wetu?

Mutiririko wa damu unaisha baada ya saa chache na kisha hapo nafasi iliyoumia inaanza kuvimba. Nafasi hiyo inapovimba, kunatokea pia mufuatano wa matukio yenye kushangaza sana. Kwanza, mishipa ya damu yenye mbele ilijifinya ili kupunguza mutiririko wa damu inatumika sasa kwa njia tofauti. Inajipanua ili kuongeza mutiririko wa damu kwenye nafasi iliyo na kidonda. Kisha, umajimaji wenye protini nyingi unafanya nafasi yote iliyo na kidonda ivimbe. Umajimaji huo ni wa maana ili kupiganisha kuambukizwa, kupunguza nguvu za sumu, na kuondoa sehemu zilizoharibika. Kila hatua inahitaji kutokeza mamilioni ya molekuli za pekee na chembe katika matukio yenye kufuatana. Zaidi ya hayo, matukio fulani kati ya matukio hayo yanachochea hatua inayofuata, na kisha hapo yanaisha.

Namna gani mwili unaendelea kujitunza?

Siku chache kisha hapo, mwili wetu unaanza kutokeza vitu vya kujitunza, utendaji huo unaonyesha mwanzo wa hatua ya tatu na unafikia mwisho katika karibu majuma mawili hivi. Chembe zinazotengeneza nyuzinyuzi ndani ya kidonda zinaingia kwenye sehemu iliyoumia na zinajifanya kuwa nyingi. Tena, mishipa midogo ya damu inatokea na kukomaa kwenye nafasi iliyoumia, na hapo inaondoa uchafu na kutokeza vitu vinavyofaa wakati wa uharibifu na wakati wa matunzo. Katika mufuatano wa matukio mengine yasiyoeleweka, chembe za pekee zinatokezwa na hilo linafanya sehemu za mwili zilizoachana zifungane.

Hiyo ni kazi nyingi kabisa! Sasa inaomba tena muda gani ili mwili umalize kujitunza?

Hatua ya mwisho ni kujirekebisha na inaweza kuchukua miezi. Mifupa iliyovunjika inarudilia nguvu yake, na nyuzi zilizowekwa kwenye eneo lenye kuregea la kidonda zinabadilishwa na vitu vyenye kuwa nguvu. Kwa ujumla, namna kidonda kinavyopona ni mufano moja wenye kushangaza wa mupangilio wa hali ya juu wenye kutumika kwa upatano.

Unaweza kukumbuka jambo moja lililokushangaza sana?

Ninapoona namna mwili unajitunza wenyewe, ninashangaa sana

Ndiyo. Ninakumbuka wakati nilimutunza kijana mwanamuke aliyekuwa na miaka 16 ambaye alifanya aksidenti mbaya sana ya motokari. Kijana huyo alikuwa katika hali mbaya sana, kiungo kimoja ndani ya tumbo yake (rate) kilikuwa kimeumia na damu ilikuwa inavuja ndani ya tumbo. Miaka ya zamani, tungemupasua na kutunza ao kutosha kiungo hicho. Leo, waganga wanaamini sana uwezo wa mwili wetu wa kujitunza wenyewe. Nilitunza tu maambukizo yake, kupunguka kwa maji ndani ya mwili, kupunguka kwa damu, na maumivu. Majuma machache kisha hapo, uchunguzi ulionyesha kwamba kiungo hicho kimepona! Ninapoona namna mwili unajitunza wenyewe, ninashangaa sana. Na hata ninaitika kabisa kwamba tuliumbwa na Mungu.

Nini ilikufanya upendezwe na Mashahidi wa Yehova?

Niliwaona kuwa wenye urafiki, na kila wakati walijibia maulizo yangu kwa kutumia Biblia. Nilipendezwa pia na namna wanaeleza imani yao bila uoga na kuwasaidia wengine wajifunze juu ya Mungu.

Kuwa Shahidi wa Yehova kulikusaidia katika kazi yako?

Ndiyo. Kwa jambo moja, kulinisaidia kupambana na hali ya kuchoka kwa sababu ya kuwahurumia watu, hali hiyo mara nyingi inawasumbua waganga ambao mara kwa mara wanatunza watu walio wagonjwa ao wanaoumia. Pia, wakati wagonjwa walipenda kuzungumuza nami, nilikuwa tayari kuwaelezea juu ya ahadi ya Muumbaji wetu ya kumaliza magonjwa na mateso *3 na kuleta dunia kwenye hakuna mutu atasema, ‘Mimi ni mugonjwa.’ *