Ona video zinazopatikana

Ni Nini Inayoweza Kukusaidia Uelewe Biblia?

Ni Nini Inayoweza Kukusaidia Uelewe Biblia?

Jibu la Biblia

 Biblia inaonyesha yale unayopaswa kufanya ili kuielewa. Hata uwe mutu wa hali gani, ujumbe wa Biblia ‘si mugumu mno kwako, wala hauko mbali.’—Kumbukumbu la torati 30:11.

Mambo unayoweza kufanya ili kuelewa Biblia

  1.   Uwe na maoni mazuri. Amini kwamba Biblia ni Neno la Mungu. Uwe munyenyekevu kwa sababu Mungu anawapinga wenye kiburi. (1 Wathesalonike 2:13; Yakobo 4:6) Hata hivyo, unapaswa kuepuka kuamini tu kila jambo unalosoma ao kusikia—Mungu anataka utumie ‘nguvu zako za kufikiri.’—Waroma 12:1, 2.

  2.   Muombe Mungu akupe hekima. Andiko la Methali 3:5,6 linasema “usitegemee uelewaji wako mwenyewe.” Tofauti na hilo, ‘endelea kumuomba Mungu” hekima ya kuelewa Biblia.—Yakobo 1:5.

  3.   Jifunze kwa ukawaida: Ili ufaidike zaidi na funzo la Biblia, unapaswa kujifunza kwa ukawaida, wala si mara chache tu.—Yoshua 1:8.

  4.   Jifunze habari moja moja. Kujifunza habari moja moja ni njia nzuri itakayokusaidia kujua yale ambayo Biblia inafundisha. Anza na “mafundisho ya mwanzo,” na kisha “usonge mbele kwa yale yaliyokomaa.” (Waebrania 6:1, 2, Habari Njema kwa Watu Wote) Utaona kwamba inawezekana kulinganisha andiko moja na andiko lingine na utatambua kwamba sehemu mbalimbali za Biblia zinasaidia kuelewa sehemu zingine, hata zile sehemu zinazozungumuzia mambo yaliyo “magumu kuelewa.”—2 Petro 3:16.

  5.   Kubali musaada. Biblia inatutia moyo tukubali musaada wa wengine wanaoelewa Biblia. (Matendo 8:30, 31) Mashahidi wa Yehova wanajifunza na watu Biblia bila malipo. Kama vile Wakristo wa kwanza-kwanza, wanatumia maandiko ili kuwasaidia wengine wajue yale ambayo Biblia inafundisha kabisa.—Matendo 17:2, 3.

Mambo ambayo hauhitaji

  1.   Akili mingi ao masomo. Mitume 12 wa Yesu walielewa Maandiko na waliyafundisha wengine, hata ikiwa watu fulani waliwaona kuwa “watu wasio na elimu na wa kawaida tu.”—Matendo 4:13.

  2.   Feza. Unaweza kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha bila kulipa. Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: ‘Mulipokea bure, toeni bure.’—Mathayo 10:8.