HABARI KUBWA | Unaweza Kuelewa Biblia
Unaweza Kupata Musaada wa Kuelewa Biblia
Wazia unatembelea inchi ya kigeni kwa mara ya kwanza. Unakuta watu, desturi, chakula, na feza zenye haujue. Kwa kweli, unaweza kujisikia kuwa mwenye kuvurugika.
Unaweza kujisikia hivyo pia wakati unasoma Biblia kwa mara ya kwanza. Unarudia nyuma katika ulimwengu wa zamani wenye kuonekana kuwa wa kigeni kwako. Huko unakuta watu wenye kuitwa Wafilisti, desturi zenye haziko za kawaida, kama vile ‘kurarua [kupasua] mavazi,’ ao unajifunza juu ya chakula chenye kuitwa mana na feza ya kichele yenye kuitwa drakma. (Kutoka 16:31; Yoshua 13:2; 2 Samweli 3:31; Luka 15:9) Mambo hayo yote yanaweza kukuvuruga. Kama vile kutembelea inchi ya kigeni, utafurahia mutu fulani akusaidie kwa kukufasiria mambo, si vile?
MUSAADA WAKATI WA ZAMANI
Kuanzia wakati maandishi matakatifu yaliandikwa kwa mara ya kwanza kati ya mwaka wa 1501 na 1600 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, watu wamepewa musaada wa kuelewa maandishi hayo. Kwa mufano, Musa, kiongozi wa kwanza wa taifa la Israeli, ‘alianza kufafanua [kufasiria]’ mambo yenye yalikuwa yameandikwa.—Kumbukumbu la Torati 1:5.
Miaka 1 000 hivi kisha hapo, kuliendelea kuwa walimu wenye kustahili kufundisha Maandiko. Katika mwaka wa 455 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, kikundi kikubwa cha Wayahudi chenye kilikuwa pia na watoto wengi, kilikusanyika pamoja mahali pa watu wengi katika muji wa Yerusalemu. Walimu wa Biblia wenye walikuwa hapo ‘walisoma kwa sauti katika kitabu [kile kile kitakatifu].’ Lakini walifanya jambo lingine. ‘Walifafanua usomaji huo.’—Nehemia 8:1-8.
Miaka 500 hivi kisha wakati huo, Yesu Kristo alifanya pia kazi kama hiyo ya kufundisha. Kwa kweli, watu walimujua kwanza kuwa mwalimu. (Yohana 13:13) Alifundisha vikundi vikubwa vya watu, na mutu mumoja-mumoja. Siku moja, alizungumuza na kikundi kikubwa cha watu, aliwafundisha mahubiri yenye kujulikana sana yenye kuitwa Mahubiri ya Mulimani, na “umati [kikundi cha watu] ukashangazwa na njia yake ya kufundisha.” (Mathayo 5:1, 2; 7:28) Katika mwaka wa 33, Yesu alizungumuza na wanafunzi wake wawili wakati walikuwa wanatembea kwenye barabara yenye kuelekea katika kijiji kimoja karibu na Yerusalemu, ‘aliwafungulia [aliwafasiria waziwazi] Maandiko’.—Luka 24:13-15, 27, 32.
Wanafunzi wa Yesu walikuwa pia walimu wa Neno la Mungu. Siku moja, mukubwa fulani Muethiopia wa nyumba ya kifalme alikuwa anasoma andiko fulani. Mwanafunzi mumoja mwenye kuitwa Filipo akamukaribia na kumuuliza hivi: ‘Unaelewa unayosoma?’ Muethiopia huyo akamujibia hivi: ‘Kwa kweli, ninawezaje kuelewa, mutu fulani asiponiongoza?’ Kisha Filipo akamufasiria maana ya andiko hilo.—Matendo 8:27-35.
MUSAADA WENYE KUPATIKANA LEO
Kama vile walimu wa Biblia wakati wa zamani, Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi ya kufundisha watu Biblia katika inchi 239 duniani pote. (Mathayo 28:19, 20) Juma kwa juma, wanasaidia watu zaidi ya milioni kenda kuelewa Biblia. Wengi kati ya watu hao wanatoka katika dini zenye haziko za Kikristo. Mutu anaweza kujifunza bila kulipa nyumbani kwake ao mahali pengine penye kumufaa. Na hata watu fulani wanafurahia kujifunza Biblia kupitia telefone ao video, kwa kutumia ordinatere ao chombo kingine cha kielektroniki.
Tafazali, zungumuza na Shahidi wa Yehova yeyote ili upate habari zaidi juu ya namna unaweza kupata faida kupitia mupango huo wa kujifunza Biblia. Utatambua kama Biblia haiko kitabu chenye hakiwezi kueleweka, lakini ni ‘yenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nizamu katika uadilifu [haki],’ ili ukuwe na ‘uwezo kamili, na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’—2 Timotheo 3:16, 17.