Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 10

Namna Gani Biblia Inaweza Kunisaidia?

Namna Gani Biblia Inaweza Kunisaidia?

SABABU GANI ULIZO HILO NI LA MAANA

Biblia inasema kwamba “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Kama jambo hilo ni kweli, Biblia inaweza kukupatia muongozo wenye uko nao lazima.

UNGEFANYA NINI?

Wazia jambo hili: David anatembeza motokari katika eneo lenye hajue hata kidogo. Alama zenye kuwa katika barabara na alama zingine zinaonyesha kwamba hakupaswa kuwa katika eneo hilo. David anatambua kama amepotea. Inawezekana katika safari yake alipita katika njia ingine yenye ilimupoteza.

Kama ungekuwa David, ungefanya nini?

WAZA KIDOGO!

Uko na mambo mengi yenye unaweza kufanya.

  1. Kutafuta muongozo.

  2. Kuchunguza karte, ao kutumia GPS (njia ya kukusaidia kujua nafasi kwenye uko ao kwenye unaenda).

  3. Kuendelea kutembeza motokari na tumaini la kwamba pengine utapata njia.

Ni wazi kama jambo la C halitakuwa na matokeo ya muzuri kabisa.

Jambo la B ni la muzuri kuliko la kwanza kwa sababu utakuwa na karte na GPS katika safari yako ili kukuongoza.

Biblia inaweza pia kukusaidia kama vile karte na GPS vinasaidia!

Kitabu hiki chenye kujulikana sana kinaweza

  • kukusaidia wakati unapata magumu katika maisha

  • kukusaidia ili ufikie kujijua muzuri na kuwa mutu muzuri

  • kukuonyesha namna ya kuwa na maisha ya muzuri zaidi

MAJIBU YA MAULIZO YA MAANA JUU YA MAISHA

Tangu wakati tunaanza kusema, tunauliza maulizo.

  • Sababu gani anga iko bleu?

  • Nyota zilitoka wapi?

Kisha tunaanza kuuliza maulizo kuhusu ulimwengu wenye kutuzunguka.

Unaweza kukubali kama majibu ya maulizo hayo yanapatikana katika Biblia tangu zamani?

Watu wengi wanasema kama Biblia inajaa hadisi za kuwazia, haina faida leo, ao kama ni nguvu kuielewa. Lakini, tatizo kabisa ni Biblia ao ni mambo yenye watu wamesikia juu ya Biblia? Watu hao wameambiwa habari za uongo?

Kwa mufano, watu wanawaza kama Biblia inasema Mungu ndiye anatawala dunia. Lakini hilo linawezekana namna gani? Dunia hii inaharibika sana! Dunia inajaa maumivu na mateso, magonjwa na kifo, umasikini na misiba. Namna gani Mungu wa upendo anaweza kuleta mambo hayo?

Unapenda kupata jibu? Mambo yenye Biblia inasema kuhusu mutu mwenye anaongoza dunia yanaweza kukushangaza!

Pengine umetambua kwamba mashauri yenye kuwa katika broshua hii yanategemea Biblia. Mashahidi wa Yehova wako hakika kwamba Biblia inatoa muongozo wenye kutumainika. Hilo ni kwa sababu Biblia ‘imeongozwa na roho ya Mungu nayo ni yenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo.’ (2 Timotheo 3:16, 17) Ni lazima uchunguze kitabu hicho cha zamani lakini chenye kingali na faida leo!