Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 28

Onyesha Shukrani Juu ya Mambo Yenye Yehova na Yesu Walikufanyia

Onyesha Shukrani Juu ya Mambo Yenye Yehova na Yesu Walikufanyia

Unajisikiaka namna gani wakati rafiki yako anakupatia zawadi ya muzuri? Unafurahiaka sana, na unapendaka kumushukuru, haiko vile? Yehova na Yesu walitupatia zawadi ya muzuri sana kupita zote. Ni zawadi gani, na unaweza kufanya nini juu ya kuwaonyesha shukrani?

1. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye Yehova na Yesu walitufanyia?

Biblia inasema kama “kila mutu mwenye anamuamini [Yesu]” anaweza kuishi milele. (Yohana 3:16) Namna gani tunaonyesha kama tunamuamini Yesu? Maamuzi yetu na matendo yetu njo inaonyesha kama tunamuamini Yesu ao hapana. (Yakobo 2:17) Wakati tunaonyesha imani kwa matendo na maneno, tunakuwa marafiki wa sana wa Yesu na wa Baba yake, Yehova.​—Soma Yohana 14:21.

2. Ni mukutano gani wa maana sana wenye unatusaidia kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye Yehova na Yesu walitufanyia?

Mangaribi mbele Yesu akufe, aliambiaka wanafunzi wake jambo ingine yenye walipaswa kufanya ili kuonyesha shukrani juu ya bei yake ya ukombozi. Alianzisha mukutano wenye Biblia inaita “Chakula cha Mangaribi cha Bwana.” Unaitwa pia Ukumbusho wa kifo ya Kristo. (1 Wakorinto 11:20) Yesu alianzisha ule mukutano juu mitume wake na Wakristo wengine wote wakuwe wanakumbuka kama alitoaka uzima wake kwa ajili yetu. Yesu alipatia wanafunzi wake hii amri: “Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (Luka 22:19) Wakati unafika ku Ukumbusho, unaonyesha kama uko mwenye shukrani juu ya upendo mukubwa sana wenye Yehova na Yesu walituonyesha.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo ingine yenye unaweza kufanya ili kuonyesha shukrani juu ya upendo mukubwa sana wenye Yehova na Yesu walituonyesha. Na tuone juu ya nini Ukumbusho wa kifo ya Yesu ni wa maana sana.

3. Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha shukrani

Waza kidogo, tuseme unatafuta kuzama. Kisha mutu fulani anakuokoa. Utasahau namna ule mutu alikuokoa? Ao utatafuta namna ya kumushukuru juu ya jambo yenye alikufanyia?

Yehova njo alitukomboa. Musome 1 Yohana 4:8-​10, kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini zabihu ya Yesu ni zawadi ya muzuri sana?

  • Unaona namna gani mambo yenye Yehova na Yesu walikufanyia?

Unaweza kufanya nini ili kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye Yehova na Yesu walitufanyia? Musome 2 Wakorinto 5:15 na 1 Yohana 4:11; 5:3. Kisha kusoma kila andiko, muzungumuzie hii ulizo:

  • Vile andiko inaonyesha, unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha shukrani?

4. Ufuate mufano wa Yesu

Jambo ingine yenye tunaweza kufanya juu ya kuonyesha shukrani, ni kufuata mufano wa Yesu. Musome 1 Petro 2:21, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani unaweza kufuata mufano ao hatua za Yesu kwa ukaribu?

5. Ufike ku Ukumbusho wa kifo ya Yesu

Juu ya kuona mambo yenye ilifanyikaka wakati Yesu alianzishaka Chakula cha Mangaribi cha Bwana, musome Luka 22:14, 19, 20. Kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Nini njo ilifanyikaka wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana?

  • Mukate inafananisha nini, na divai inafananisha nini?​—Ona mustari wa 19 na 20.

Yesu alipenda wanafunzi wake wakuwe wanafanya Ukumbusho wa kifo yake kila mwaka. Alipenda wakuwe wanafanya vile tarehe yenye alikufaka. Mashahidi wa Yehova wanatii ile amri ya Yesu. Njo maana, kila mwaka wanakutanaka pamoja juu ya kufanya Ukumbusho wa kifo ya Kristo. Juu ya kujua mambo mingi zaidi juu ya ule mukutano wa maana sana, muangalie VIDEO. Kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Nini njo inafanyikaka ku Ukumbusho?

Mukate na divai ni mifano. Mukate unafananisha mwili mukamilifu wa Yesu wenye alitoa kwa ajili yetu, na divai inafananisha damu yake

WATU FULANI WANASEMAKA: “Kama tu unaamini Yesu, utaokolewa.”

  • Namna gani unaweza kutumia Yohana 3:16 na Yakobo 2:17 ili kuonyesha kama zaidi ya kuamini Yesu, kuko mambo ingine yenye mutu anapaswa kufanya?

KWA KIFUPI

Tunaonyesha shukrani juu ya mambo yenye Yesu alitufanyia kwa kumuamini na kufika ku Ukumbusho wa kifo yake.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Unaweza kuonyesha namna gani kama unamuamini Yesu?

  • Utafanya nini juu ya kuonyesha kama uko mwenye shukrani juu ya mambo yenye Yehova na Yesu walikufanyia?

  • Juu ya nini ni muzuri ukuwe nafika ku Ukumbusho wa kifo ya Yesu?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Kifo ya Yesu inatuchochea kufanya nini?

Alitumia Mwili Wake Juu ya Kumuletea Yehova Utukufu (9:28)

Ujifunze mambo mingi zaidi juu ya imani na namna unaweza kuionyesha.

“Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 10, 2016)

Mu habari yenye kichwa “Sasa Niko Safi na Ninafurahia Maisha,” ona namna kujifunza juu ya zabihu ya Kristo kulisaidia mwanamuke fulani.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 8, 2011)

Ona juu ya nini ni watu kidogo tu njo wanakulaka mukate na kunywa divai ku Ukumbusho.

“Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Wanafanyaka Meza ya Bwana Tofauti na Dini Zingine?” (Inapatikana ku Enternete)