Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 12

Nini Njo Inaweza Kukusaidia Uendelee Kujifunza Biblia?

Nini Njo Inaweza Kukusaidia Uendelee Kujifunza Biblia?

Kujifunza Biblia iko na faida. Lakini, wakati fulani, haikuwake mwepesi. Unaweza kujiuliza kama utaweza kuendelea kujifunza Biblia. Utapata faida gani kama unajikaza kuendelea kujifunza? Nini njo inaweza kukusaidia usiache hata kama unapata magumu?

1. Juu ya nini ni muzuri ujifunze Biblia?

“Neno la Mungu liko na uzima na liko na nguvu.” (Waebrania 4:12) Ni muzuri ujifunze Biblia juu inatusaidia kujua mawazo ya Mungu na kujua kama anatupenda. Inatusaidia tujue mambo mingi, tukuwe na hekima ya kweli na tumaini. Zaidi ya yote, Biblia inatusaidia tukuwe marafiki wa Yehova. Kama unajifunza Biblia, itakusaidia ukuwe na maisha ya muzuri.

2. Kuona mafundisho ya Biblia kuwa ya maana kutakusaidia namna gani?

Kweli yenye iko mu Biblia, ni kusema mafundisho ya Biblia, ni ya maana sana. Njo maana Biblia inatuambia hivi: “Ununue kweli na usiiuzishe hata kidogo.” (Mezali 23:23) Kuona mafundisho ya Biblia kuwa ya maana kutakusaidia ufanye yako yote juu uendelee kujifunza, hata kama kunakuwa mambo yenye inaweza kufanya uache.​—Soma Mezali 2:4, 5.

3. Namna gani Yehova anaweza kukusaidia uendelee kujifunza?

Yehova, Muumbaji wako mwenye nguvu na Rafiki yako, anapenda kukusaidia uendelee kujifunza juu yake. Anaweza kukupatia “hamu na pia nguvu za kutenda.” (Soma Wafilipi 2:13.) Njo maana, kama wakati fulani unajisikia uko na lazima ya mutu wa kukupatia hamu zaidi ya kujifunza na kutumikisha mambo yenye uko unajifunza, Mungu anaweza kukusaidia. Tena, Mungu anaweza kukupatia nguvu zaidi ya kuvumilia magumu ao ya kuvumilia wakati wengine wanajaribu kukukataza kujifunza Biblia. Ukuwe unamuomba Yehova akusaidie juu uendelee kujifunza.​—1 Watesalonike 5:17.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye inaweza kukusaidia uendelee kujifunza hata kama uko na mambo mingi ya kufanya, ao kama wengine wako wanakukataza kujifunza Biblia. Kisha, tuone namna Yehova atakusaidia uendelee kujifunza.

4. Uone kujifunza Biblia kuwa jambo ya maana sana

Tunaweza kuwa na mambo mingi ya kufanya mupaka tunaanza kuwaza kama hatuna wakati ya kujifunza Biblia. Kama ni vile, nini njo inaweza kutusaidia? Musome Wafilipi 1:10, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unawaza “mambo ya maana zaidi” mu maisha njo mambo gani?

  • Namna gani unaweza kuonyesha kama unaona kujifunza Biblia kuwa jambo ya maana sana?

  1. Kama unatia muchanga mu mbeketi kisha njo unaongeza majiwe, majiwe haitapata fasi

  2. Kama unatia kwanza majiwe, muchanga haitakosa fasi. Vilevile, kama unafanya kwanza “mambo ya maana zaidi,” utapata wakati ya kufanya mambo ingine

Kujifunza Biblia kunatimiza uhitaji wetu wa kiroho, ni kusema hamu yetu ya kumujua Mungu na kumuabudu. Musome Matayo 5:3, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Tunapata faida gani wakati tunaona kujifunza Biblia kuwa jambo ya maana sana?

5. Usiache kujifunza hata kama watu wanakukataza

Wakati fulani, wengine wanaweza kukuambia uache kujifunza Biblia. Tuone mufano wa Francesco. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, marafiki na watu wa familia ya Francesco walifanya nini wakati aliwaambia mambo yenye iko najifunza?

  • Alipata baraka gani juu hakuacha?

Musome 2 Timoteo 2:24, 25, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Marafiki na watu wa familia yako wanaonaka namna gani mambo yenye uko najifunza?

  • Vile ile andiko inaonyesha, unapaswa kufanya nini kama mutu fulani hafurahie kuona namna uko najifunza Biblia? Juu ya nini?

6. Yehova atakusaidia

Wakati urafiki wetu na Yehova unaendelea kuwa nguvu, ni vile tutapenda sana kumufurahisha. Hata vile, wakati fulani tunaweza kuona kama ni nguvu kuachana na tabia zenye Yehova hapendake. Kama unaona vile, usivunjike moyo. Yehova anaweza kukusaidia. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, Jim aliachana na tabia gani juu amufurahishe Yehova?

  • Nini njo inafanya ufurahie mufano wake?

Musome Waebrania 11:6, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yehova atafanyia nini wale wenye “wanamutafuta kwa bidii,” ni kusema, wenye wanajikaza kumujua na kumufurahisha?

  • Ile inaonyesha kama Yehova anajisikiaka namna gani wakati anaona uko najikaza kujifunza Biblia?

KAMA MUTU ANAULIZA: “Juu ya nini uko najifunza Biblia?”

  • Utamujibia nini?

KWA KIFUPI

Wakati fulani haikuwake mwepesi kujifunza Biblia. Lakini, kufanya vile kunaweza kukusaidia ufurahie maisha milele. Uendelee kumuomba Yehova akusaidie, na atakubariki.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini unaona mafundisho ya Biblia kuwa ya maana?

  • Namna gani unaweza kuonyesha kama unaona kujifunza Biblia kuwa jambo ya maana?

  • Juu ya nini unapaswa kumuomba Yehova akusaidie uendelee kujifunza Biblia?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona mambo ine yenye imesaidia watu wengi watumie muzuri wakati yao.

“Namna ya Kutumia Wakati Wako kwa Hekima” (Amuka!, Mwezi wa 2, 2014)

Ona namna Yehova alisaidia mwanamuke fulani mwenye bwana yake hakufurahia kuona namna alikuwa anajikaza kufurahisha Mungu.

Yehova Anatutia Nguvu ili Tuweze Kubeba Muzigo Wetu (5:05)

Ona namna mwanaume fulani alipata faida juu bibi yake hakuacha kujifunza.

Nilipenda Kujua Ikiwa Mafundisho ya Biblia Ni ya Kweli Kabisa (6:30)

Wakati fulani, watu wanasemaka kama Mashahidi wa Yehova wanavurugaka familia za watu. Ile ni kweli?

“Mashahidi wa Yehova Wanavurugaka Familia za Watu ao Wanazisaidiaka Zikuwe Nguvu?” (Inapatikana ku Enternete)