Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Sababu gani amani imekosekana kabisa duniani?

Ni serikali tu inayoweza kubadilisha mioyo ya watu ndiyo italeta amani duniani

Biblia inaonyesha sababu mbili. Sababu ya kwanza, hata ikiwa wanadamu wametimiza mambo ya ajabu, hawakuumbwa wakiwa na uwezo wa kuongoza hatua zao wenyewe. Sababu ya pili, mipango ya wanadamu imeshindwa kwa sababu ‘ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za yule muovu,’ Shetani Ibilisi. Kwa hiyo, hata ikiwa wanadamu wamejikaza sana, hawajaweza kuleta amani duniani.​—Soma Yeremia 10:23; 1 Yohana 5:19.

Hali ya wanadamu ya kutafuta faida zao wenyewe na kutafuta mambo makubwa imefanya pia amani ikosekane kabisa duniani. Serikali moja tu ya duniani pote ambayo inaweza kufundisha watu kupenda mema na kuhangaikiana ndiyo italeta amani duniani.​—Soma Isaya 32:17; 48:18, 22.

Ni nani atakayeleta amani duniani?

Mungu Mweza-Yote ameahidi kuweka serikali moja tu duniani ili itawale wanadamu wote. Serikali hiyo itachukua nafasi ya serikali za wanadamu. (Danieli 2:44) Yesu, Mwana wa Mungu, atatawala akiwa Mukubwa wa Amani. Ataondoa mambo yote maovu duniani na atafundisha watu njia ya amani.​—Soma Isaya 9:6, 7; 11:4, 9.

Hata leo, chini ya uongozi wa Yesu, mamilioni ya watu duniani wanatumia Neno la Mungu, Biblia, ili kufundisha watu namna ya kuishi kwa amani pamoja na wengine. Hivi karibuni, amani itapatikana kabisa duniani.​—Soma Isaya 2:3, 4; 54:13.