Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Ulijua?

Je, Ulijua?

Je, Ulijua?

Majiwe ya bei sana yaliyotiwa kwenye mufuko wa kifuani wa vazi la kuhani mukubwa wa Israeli yalitoka wapi?

Baada ya Waisraeli kutoka Misri na kuingia katika jangwa, Mungu aliwaagiza wafanye mufuko huo wa kifuani. (Kutoka 28:15-21) Mufuko huo ulikuwa na jiwe la zabarijadi, topazi, zumaridi, feruzi, yakuti, yaspi, leshemi, akiki, ametisti, krisolito, shohamu, na yashefi. * Namna gani Waisraeli wangeweza kupata majiwe hayo ya bei sana?

Wakati wa zamani, watu waliona majiwe hayo kuwa ya bei sana na pia waliyafanyia biashara. Kwa mufano, wakaaji wa zamani wa Misri (Egypte) walinunua majiwe hayo mbali sana kama vile huko Iran ya leo, Afghanistan, na labda hata Inde. Huko Misri, kulikuwa majiwe mbalimbali ya bei sana. Wafalme wa Misri ndio waliokuwa na haki ya kuchimbua majiwe ya bei sana katika maeneo yote waliyokuwa wakitawala. Ayubu alieleza namna watu wa wakati wake walivyochimba mashimo katika udongo ili kutafuta majiwe ya bei sana. Ayubu alitaja hasa yakuti na topazi kati ya majiwe hayo yaliyochimbwa katika udongo.​—Ayubu 28:1-11, 19.

Kitabu cha Kutoka kinaeleza kama Waisraeli, walipotoka Misri, walichukua vitu vya bei sana vya Wamisri, “wakawaacha Wamisri bila chochote.” (Kutoka 12:35, 36) Kwa hiyo, inawezekana Waisraeli walipata huko Misri majiwe yaliyotiwa kwenye mufuko wa kifuani wa vazi la kuhani mukubwa.

Sababu gani divai ilitumiwa kama dawa wakati wa zamani?

Katika moja ya mifano yake, Yesu alizungumuzia mutu aliyepigwa na wanyanganyi. Yesu alisema kama mutu huyo alisaidiwa na Musamaria aliyefunga vidonda vyake na kumuangia “mafuta na divai juu yake.” (Luka 10:30-34) Paulo alipomuandikia rafiki yake Timotheo, alimushauria hivi: “Usiendelee kunywa maji, bali utumie divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako na ugonjwa wako wa mara kwa mara.” (1 Timotheo 5:23) Tabia ambayo Yesu alieleza ya kumuangia divai kwenye vidonda na shauri ambalo Paulo alimupatia Timotheo, je, vinapatana kabisa na mambo ya kiganga?

Kitabu fulani (Ancient Wine) kinaeleza kama divai ni “dawa ya kutuliza maumivu, ni dawa ya kuua mikrobe, na ni dawa ya magojwa mengi.” Wakati wa zamani, wakaaji wa Misri, wakaaji wa Mesopotamie, na wakaaji wa Syrie walitumia sana divai katika matunzo. Kitabu fulani (The Oxford Companion to Wine) kinaeleza kama divai ni “dawa ambayo imemusaidia mwanadamu tangu wakati wa zamani.” Kupatana na shauri ambalo Paulo alimupatia Timotheo, kitabu fulani (The Origins and Ancient History of Wine) kinasema hivi: “Kisha kupima, imeonekana kama mikrobe ya homa ya matumbu (typhoïde) na mikrobe mingine mingi iliyo hatari inakufa haraka inapotiwa katika divai.” Uchunguzi wa sasa unahakikisha kama kati ya sehemu zinazofanyiza divai, zaidi ya sehemu 500 zina uwezo wa kutunza magonjwa mbalimbali.

[Maelezo ya chini]

^ Ni vigumu kujua namna majiwe hayo yanaitwa leo.

[Picha katika ukurasa wa 26]

Picha ya watu wa hali ya chini wanaokanyanga​-kanyanga mizabibu, ilichukuliwa kwenye kaburi la Nakht, Thebes, huko Misri

[Picha zimetolewa na]

Gianni Dagli Orti/The Art Archive at Art Resource, NY