Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wazazi—Muwazoeze Watoto Wenu Tangu Utoto Muchanga

Wazazi—Muwazoeze Watoto Wenu Tangu Utoto Muchanga

BIBLIA inasema hivi: ‘Tazama! Wana ni uriti kutoka kwa Yehova; uzao wa tumbo ni zawabu.’ (Zab. 127:3) Kwa hiyo, haishangaze kuona wazazi Wakristo wakifurahi sana wanapopata mutoto.

Kuzaliwa kwa mutoto kunaleta furaha lakini pia madaraka mazito. Ili mutoto afikie kuwa mutu muzima mwenye afya nzuri, anahitaji kula chakula kizuri kila siku. Vivyo hivyo, ili mutoto ashikamane na ibada ya kweli, anahitaji chakula kizuri cha kiroho na muongozo kutoka kwa wazazi wanaojikaza kumufundisha kanuni za Mungu. (Met. 1:8) Mazoezi hayo yanapaswa kuanza wakati gani na yanapaswa kutia ndani nini?

WAZAZI WANAHITAJI MAAGIZO

Fikiria Manoa aliyekuwa wa kabila la Dani, na aliyeishi katika muji wa Sora katika Israeli. Malaika wa Yehova alimuelezea bibi ya Manoa, aliyekuwa tasa, kwamba angezaa mwana. (Amu. 13:2, 3) Mwanaume huyo mwaminifu na bibi yake walitazamia kwa furaha sana kupata mutoto. Hata hivyo, kuna mambo ambayo yaliwahangaisha. Kwa hiyo Manoa alisali hivi: ‘Nakuomba razi, Yehova. Tafazali, yule mutu wa Mungu wa kweli ambaye ulimutuma na arudi kwetu tena, atufundishe yale tunayopaswa kumutendea huyo mutoto atakayezaliwa.’ (Amu. 13:8) Manoa na bibi yake walitafuta kujua namna gani wangemulea mutoto wao. Bila shaka, walimufundisha mwana wao Samsoni, sheria ya Mungu, na walipata matokeo mazuri. Biblia inasema hivi: ‘Baada ya muda roho ya Yehova ikaanza kumuchochea [Samsoni].’ Matokeo yalikuwa mazuri kwa sababu mwamuzi Samsoni alifanya mambo mengi ya ajabu.​—Amu. 13:25; 14:5, 6; 15:14, 15.

Manoa alisali ili kupata uongozi kuhusu namna ya kumulea mutoto ambaye angezaliwa

Wazazi wanapaswa kuanza kuzoeza mutoto wao tangu wakati gani? Eunike, mama ya Timotheo, na Loisi, tate ao kambo yake walimuzoeza katika “maandishi matakatifu” ‘tangu utoto muchanga.’ (2 Tim. 1:5; 3:15) Bila shaka, Timotheo alianza kuzoezwa kupitia Maandiko tangu utoto muchanga.

Ni jambo la hekima wazazi Wakristo wasali ili kupata muongozo na kufanya mipango mbele ya wakati ili waweze kumuzoeza mutoto wao tangu ‘utoto muchanga.’ Methali 21:5 inasema hivi: “Mipango ya mwenye bidii bila shaka huleta faida.” Mbele mutoto azaliwe, bila shaka wazazi watajitayarisha vizuri. Wanaweza hata kuandika mambo ambayo mutoto huyo atahitaji. Ni jambo la lazima pia wafikirie namna watakavyomuzoeza kiroho. Muradi wao unapaswa kuwa kuanza kumuzoeza akiwa angali muchanga.

Kitabu Early Childhood Counts​—A Programming Guide on Early Childhood Care for Development kinasema hivi: “Miezi ya kwanza-kwanza kisha mutoto kuzaliwa ni wakati wa maana sana kuhusiana na ukomavu wa ubongo. Katika kipindi hicho sinapsi ao njia za kupitishia habari katika ubongo zinaongezeka mara 20.” Ni jambo la hekima kabisa wazazi watumie kipindi hicho kifupi cha wakati ili kuingiza katika akili ya mutoto wao mawazo ya kiroho na kanuni za Mungu!

Mama mumoja, ambaye ni painia wa kawaida, alisema hivi kuhusu binti wake mudogo: “Nimekuwa nikienda naye katika mahubiri tangu alipokuwa tu na umri wa mwezi moja. Hata ikiwa hakuelewa jambo lolote, niko hakika kwamba kumupeleka katika mahubiri akiwa na umri mudogo hivyo kulikuwa na matokeo mazuri sana juu yake. Alipokuwa na umri wa miaka miwili, alitolea watu tuliokutana nao katika mahubiri trakti bila woga.”

Kila mara kuzoeza mutoto tangu umri mudogo sana kunaleta matokeo mazuri. Lakini, wazazi wanajua kwamba si rahisi kuwatolea watoto wao mazoezi ya kiroho.

‘MUJINUNULIE WAKATI UNAOFAA’

Kukosa utulivu kwa mutoto na uwezo wake mudogo wa kukazia uangalifu mambo kunaweza kufanya iwe vigumu sana kwa wazazi kumuzoeza. Akili ya watoto inaweza kutanga​-tanga kwa sababu wanapenda kuuliza​-uliza na wanapenda kujua vitu vinavyowazunguka. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kusaidia watoto wao wakazie uangalifu mambo wanayojaribu kuwafundisha?

Fikiria yale ambayo Musa alisema. Andiko la Kumbukumbu la Torati 6:6, 7 linasema hivi: ‘Maneno haya ninayokuamuru leo lazima yawe moyoni mwako; nawe uyakazie kwa mwana wako na kuyasema unapoketi katika nyumba yako na unapotembea barabarani na unapolala na unapoamuka.’ Neno “uyakazie” linamaanisha kufundisha kwa kurudilia-rudilia. Mutoto muchanga anaweza kufananishwa na muti mudogo unaopaswa kumwangiwa maji kwa ukawaida. Kwa kuwa kurudilia mambo kunasaidia watu wazima wakumbuke mambo ya lazima, njia hiyo itawasaidia kabisa watoto wachanga!

Ili kufundisha watoto ukweli ni lazima wazazi wapitishe wakati pamoja nao. Katika ulimwengu wa leo wenye shuguli nyingi, inaweza kuwa vigumu kupata wakati wa kufundisha watoto. Lakini mutume Paulo alitushauri ‘tujinunulie wakati unaofaa’ kwa ajili ya mambo kiroho. (Efe. 5:15, 16) Tunaweza kufanya hivyo namna gani? Muzee mumoja wa kutaniko, ambaye bibi yake ni painia aliye na mengi ya kufanya, alishindwa kusawazika kati ya kufundisha mutoto wao, kushugulikia madaraka katika kutaniko, na kufanya kazi ya kimwili. Namna gani wangepata wakati wa kumuzoeza binti yao? Baba anasema hivi: “Kila asubuhi mbele ya kwenda kwenye kazi, bibi yangu nami tunamusomea mutoto wetu habari fulani katika kitabu Hadithi za Biblia ao kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku. Mangaribi, tunahakikisha kwamba tulimusomea habari fulani mbele alale, na tunapoenda katika mahubiri, tunaenda pamoja naye. Hatupendi kukosa wakati wa kumuzoeza katika miaka hiyo ya kwanza-kwanza ya maisha yake.”

‘WANA NI KAMA MISHALE’

Bila shaka, tunapenda watoto wetu wakomae na kuwa watu wenye kuchukua mambo kwa uzito. Lakini, sababu ya kwanza inayotuchochea tuwazoeze ni kuingiza upendo wa Mungu katika mioyo yao.​—Mk. 12:28-30.

Zaburi 127:4 inasema hivi: ‘Kama mishale mukononi mwa mwanaume mwenye nguvu, ndivyo walivyo wana wa ujanani.’ Kwa hiyo, watoto wanafananishwa na mishale inayopaswa kulengwa vizuri ili kufikia shabaha. Kisha kuutupa mushale, mupiga-mishale hawezi tena kuurudisha nyuma. Wazazi wana “mishale,” ni kusema, watoto wao kwa kipindi kidogo tu cha wakati. Kwa hiyo, wanapaswa kutumia wakati huo ili kuingiza kanuni za Mungu katika akili na mioyo ya watoto wao.

Kuhusu watoto wake wa kiroho, mutume Yohana aliandika hivi: “Sina sababu nyingine kubwa zaidi ya kuwa na shukrani kuliko mambo haya, kwamba niwe nikisikia watoto wangu wanaendelea kutembea katika kweli.” (3 Yoh. 4) Wazazi Wakristo wanaweza pia kusema hivyo wanapoona watoto wao ‘wakiendelea kutembea katika kweli.’