Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Jina Lenye Kuwa Katika Biblia Linapatikana Kwenye Mutungi wa Zamani

Jina Lenye Kuwa Katika Biblia Linapatikana Kwenye Mutungi wa Zamani

Katika mwaka wa 2012, wachimbuaji wa vitu vya zamani walivumbua vipande vya mutungi wenye kutengenezwa na udongo vyenye viko na miaka 3000. Watu wenye kutafuta habari walifurahi sana. Sababu gani? Haiko kwa sababu ya vipande vya mutungi huo lakini kwa sababu ya maandishi yenye yalikuwa kwenye vipande hivyo.

Wakati wachimbuaji wa vitu vya zamani waliweka vipande vyote pamoja, waliweza kusoma maandishi fulani ya Wakanaani kwenye mutungi huo. Yalisema hivi: “Eshba’al Ben Beda,” maana yake, “Eshba’al, mutoto mwanaume wa Beda.” Hiyo ni mara ya kwanza wachimbuaji wa vitu vya zamani wamevumbua jina hilo lenye kuandikwa kwenye chombo fulani cha zamani.

Biblia inazungumuzia mutu mwengine mwenye kuitwa Eshbaali. Alikuwa mumoja kati ya watoto wanaume wa Mufalme Sauli. (1 Mambo ya Nyakati 8:33; 9:39) Profesa Yosef Garfinkel, mutu mumoja kati ya wale wenye walivumbua mutungi huo, alisema hivi: “Ni jambo lenye kufurahisha kuona kwamba jina Eshba’al linapatikana katika Biblia, wakati wa utawala wa Mufalme Daudi tu, na sasa pia katika habari za vitu vya zamani vyenye vimechimbuliwa.” Huu ni mufano mwengine wenye kuonyesha kuwa habari za vitu vya zamani vyenye vimechimbuliwa zinaunga Biblia mukono!

Katika Biblia, Eshbaali, mutoto mwanaume wa Sauli anaitwa pia Ish-boshethi. (2 Samweli 2:10) Sababu gani neno “baali” lilibadilishwa na neno “boshethi”? Wachunguzi wanasema kuwa pengine muandikaji wa kitabu cha Pili cha Samweli aliepuka kutumia jina Eshbaali kwa sababu lilikumbusha Waisraeli Baali, mungu wa upepo mukali mwenye Wakanaani walikuwa wanaabudu. Hata hivyo, jina Eshbaali linaendelea kupatikana katika kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati.